Monday, July 20, 2009

Mnorweji wa kwanza afariki

kwa mafua ya nguruwe



Mnorwejiani mwanamme wa miaka 29 amefariki kwa homa ya nguruwe akiwa kwenye Jamhuri ya Dominika juzi Jumamosi TV 2 ya Norway imetangaza. Hayo yamethibitishwa na Bi. Marte Koppstad, msemaji wa wizara ya mambo ya nchi za nje mjini Oslo. Jamaa huyo alikuwa likizo na mshkaji wake, aliposhikwa na mafua, baadaye akaishiwa na nguvu na kupoteza fahamu na hakuamka tena. Kwa tahadhari zaidi kuhusu mafua ya nguruwe bofya na soma melezo toka Shirika la Afya Duniani (WHO)

No comments: