Monday, September 24, 2007

Ray C: Promota kaniyeyusha

Ile Tour iliyotangazwa saana na kuzua gumzo mjini kuwa Ray C kapata deal la nguvu la kuzunguka mabara kadhaa duniani limeenda ndivyo sivyo.
Akielezea sakata hilo mwanadada machachari jukwaani alisema kuwa promota alimyeyusha hivyo amekatisha tour yake nayupo around

....Unajua nilimuamini promota na sikuchukua advance ndilo kosa nililofanya katikati ya tour nikagundua jamaa ni longo longo kulikuwa hakuna mpangilio wowote wa tour hiyo licha ya kuitangaza vya kutosha......alisema Ray czzzzooo

Ray c alisema, alianza kuzinguana na promota baada ya kupiga kama show nne hivi alipotaka mapene ndipo jamaa alipoleta miyeyusho na kuamua kuua dili nakurudi zake home

Tour hiyo ilikuwa imeandaliwa na kampuni ya George Inc ambayo Ray C aliongozana na msanii kutoka kundi la Nako2Nako lenye maskani yake Arusha.

Habari hizi kutoka: DarHotWire.


No comments: