Friday, December 28, 2018
Wednesday, December 12, 2018
Kwa Watanzania na wenye nasaba na asili
ya Tanzania duniani
Tunapenda
kukujulisha kuwepo kwa Baraza la Diaspora kwa Watanzania Duniani. Lengo la
Baraza ni kuwaunganisha diaspora wote wa Kitanzania ktk taasisi moja ili
kupata taarifa mbalimbali zinazowahusu diaspora wa Tanzania kwa haraka na
kushauriana kuhusu mahitaji ya diaspora na jinsi ya kuyatetea. Kupata
taarifa hizo bonyeza Link hii
Kujiunga
na Baraza bonyeza link hii http://www.tdcglobal.org/member-register/
Karibu
sana
NB:Ukipatwa
na tatizo lolote kwenye kujiunga piga simu
+47 46 21
86 09
Ukipata
taarifa hii mjulishe na mwenzako.
Agnes Lerdorf
Kamati ya Mahusiano na Umma
Tanzania
Global Diaspora Council
Pamoja
Tunaweza - Mtu Kwao Ndio Ngao
Monday, December 10, 2018
Friday, December 07, 2018
Wednesday, March 21, 2018
Kutoka ubalozini Stockholm kuhusu vitambulisho vya taifa na pasipoti mpya

Kwa Viongozi wa Jumuiya ya Watanzania,
(NIDA) kuhusu usajili wa Watanzania waishio nje ya nchi (Diaspora).
+255 713 412 871
UBALOZI WA TANZANIA
KWENYE NCHI ZA NORDIC
NA ZA BALTIC
STOCKHOLM.
SWEDEN
http://www.tanemb.se
Wednesday, February 21, 2018
Sunday, February 18, 2018
YAHUSU UTARATIBU WA MAOMBI YA PASIPOTI MPYA YA KIELETRONIKI YA TANZANIA
KWA WAOMBAJI WA NDANI NA NJE YA TANZANIA
Ubalozi wa Tanzania Sweden umepokea maelezo toka Wizara ya Mambo ya Ndani, Idara ya Uhamiaji juu ya utaratibu wa maombi ya pasipoti mpya kama ifuatavyo:
"Idara ya Uhamiaji imeanza kutoa Pasipoti mpya za kielektroniki kwa Watanzania kuanzia tarehe 31. Januari 2018.
Pasipoti za zamani zitaendelea kuwa halali kwa matumizi hadi ifikapo tarehe 31.Januari 2020.
Utaratibu mpya wa maombi kwa sasa utawahusu waombaji wa pasipoti waliopo ndani ya nchi tu.
Kwa waombaji waliopo nje ya nchi wataendelea na utaratibu wa zamani na kupewa pasipoti za zamani mpaka hapo mitambo ya kuchukua alama za vidole itakaposimikwa kwenye balozi zetu".
Hivyo kwa taarifa hii watanzania mnaoishi nchi za Nordic na Baltic mtaendelea kutumia pasi mlizonazo na mkiomba mpya mtapata kama hizi za zamani mpaka hapo ubalozi utakapowezeshwa kupokea maombi ya pasi mpya.
Ukipata taarifa hii mwambie na mwingine!
MATIKU KIMENYA,
KAIMU BALOZI
UBALOZI WA TANZANIA
NCHI ZA NORDIC NA
ZA BALTIC,
STOCKHOLM
SWEDEN.
Thursday, October 12, 2017
Wednesday, October 04, 2017
Saturday, August 19, 2017
Tunasikitika kutangaza kifo cha Sadiki Rajabu Bulibha,
kilichotokea Oslo, Norway Jumatano, 16. Agosti 2017
Mwili wa marehemu uko hospitali kwa uchunguzi utakaofanyika kati ya Jumatatu na Jumatano wiki ijayo.
Chama Cha Watanzania Oslo kitawataarifu mipango ya mazishi wiki ijayo.
Mwenyezi Mungu Amlaza Pema, Ameen!
Sunday, April 30, 2017
Tuesday, April 18, 2017
Friday, March 31, 2017
Thursday, March 30, 2017
Friday, March 24, 2017
Tuesday, March 21, 2017
Sunday, March 19, 2017
Friday, March 17, 2017
Friday, March 10, 2017
Polisi Dar es Salaam wameongea kuhusu kukamatwa kwa Vanessa Mdee - Kamishna wa Polisi kanda maalum ya Dar es salaam Simon Sirro leo Machi 10, 2017 amekutana na waandishi wa habari na kutoa taarifa kuhusu zoezi linaloendelea la ukamataji wa watuhumiwa wa dawa za kulevya ambapo amethibitisha kuwa wamemkamata mwimbaji Vanessa Mdee ni baada ya kutajwa kwenye orodha ya mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda
Wednesday, March 01, 2017
Tuesday, February 28, 2017
Mazishi ya Marehemu Abdallah Khelef Shauri "Dullah" Nchini Norway jana Jumatatu 27.Februari 2017
Sofia Abdallah Khelef Shauri (mtoto wa marehemu Abdallah Khelef Shauri) akiweka shada la maua la uchungu katika kaburi la baba yake baada ya kuzikwa jana.
Familia ya Shauri Mjaka na ndugu zake inatowa shukrani kwa Wananchi Wote walioshiriki kwa njia moja kuungana na familia hiyo katika kipindi chote cha msiba wa mtoto wao Abdallah Khefel Shauri «Dullah» katika kipindi kigumu cha msima huo uliotokea nchini Norway siku ya Jumamosi iliopita na kufikia tamati ya kukamilisha shughuli za mazishi zilizofanyika jana nchini Norway katika majira ya mchana saa 6:00 kwa kuuhifadhi mwili wa marehemu kwa kukamilisha taratibu zote za mazishi, Skoger Drammen.
Tunatoa shukrani kwa mzazi mwenziwe Mama Sofia kwa mchango mkubwa aliotoa kufanikisha maziko hayo. Tunatoa shukrani za dhati kwa Mama Sofia Inshaallah Mwenyenzi Mungu atakujalia kila la kheri katika maisha yako.
Pia na marafiki waliofika kutoka nchi jirani na kuwahi msiba huo kumshindikia
mpendwa rafiki yao.
Inatowa shukrani kwa Jumuiya zote za Watanzania wanaoishi nje kwa umoja wao kwa hali na mali kuweza kufanikisha suala hii kwa ushirikiano wao. Tunatoa shukrani kwa uongozi wa Jumuiya watanzania Wanaoishi nchini Norway kusimamia suala hili hadi mwisho kufanya taratibu za mazishi ya Ndugu yetu. Tunatoa Shukrani kwa Jumuiya ya Kiislamu ya Watanzania Norway na Ndugu Hassan na Jamal kusimamia hadi kukamilika.
Hatuna cha kuwalipa kwa hili inshalla Mwenyenzi Mungu atawajalia kila la kheri na moyo wa imana kwa hili na lengine.
Ameen.
Tuesday, February 21, 2017
Subscribe to:
Posts (Atom)