Ugonjwa uliomuua Amina!
Ugonjwa huu mpya ambao aliugua Bi. Chifupa na uliosababisha mauti  yake kwa jina la kitaalamu hujulikana kama Uumbuajiasis Viongozitanzanialitis  Hadharanum.Ugonjwa huu unatokana na kufuatilia mambo ya serikali na  viongozi kwa karibu kiasi cha kutaka kuweka ubovu wao hadharani.
Dalili kubwa za ugonjwa huu ni hizi:   
a. Kupenda nchi zaidi kuliko chama   
b. Kuwa tayari kutetea mali ya Taifa na kuilinda mali hiyo   
c. Kutoogopa yatakayokukuta karibu
d. Kuanza kuweka hadharani ubovu na siri za viongozi hasa kwa jamaa yako wa karibu
e. Kutosikiliza ushauri wa kutakiwa kukaa kimya na wakubwa wako   
f. Kuwa kimbelembele kuzungumza na kukemea maovu kila upatapo nafasi   
g. Kuwa mtetezi wa Katiba na mkosoaji wa jamii   h. Kutolegeza msimamo hadi kifo.   
Maambukizi:   Ugonjwa huu unaambukiza watu wachache kwani watu wengi wameshapatiwa  kinga yake. Kwa wale wanaombukizwa wanafanya hivyo zaidi kwa kusoma habari  za ufisadi, rushwa, na ubadhirifu katika serikali yao. Kwa
kupitia  mitandao, vitabu, na vyombo vya habari virusi vya ugonjwa huu vinajipenyeza  katika akili za watu na kusababisha kusisimka kwa ubongo. Wale  waliombukizwa ugonjwa huu hujikuta wakitafuta habari za kila namna  na kushiriki mijadala yenye kutafakari mustakabali wa Taifa lao.   
Kinga:   Ugonjwa huu kinga yake kubwa hujulikana kwa kitaalamu kama Mrungura.  Kinga hii hutolewa kwa wale wote wenye kuanza kuonesha dalili za kukumbwa  na ugonjwa huu. Kinga hii huwekwa kwenye mabenki na maofisi  mbalimbali ili kuzuia viongozi wakubwa wasipatwe na virusi vya ugonjwa huu. Kinga hii pia hufanya kazi kwa wale walioanza kuonesha dalili kama kina Phillip Marmo, Chrisant Mzindakaya n.k Pindi mtu akishapatiwa kinga hii  HAWEZI kuipinga serikali!   
Tiba:   Hadi hivi sasa ugonjwa huu hauna tiba ya uhakika kwani wale ambao  wameshaugua kwa muda mrefu hawako tayari kutibiwa kwani wanaona  wanaishi vizuri tu na ugonjwa huu.   
Karantini:   Pindi baadhi ya wakubwa wakiona kuna mtu ambaye amefikia hatua ya  juu kabisa ya ugonjwa huu basi kwa mbinu wanazozijua wenyewewanamkarantini, na wakati mwingine anakuwa katika hali hiyo ya  kutengwa hadi kifo ili asiendelee kuwaambukiza watu wengine.   Jihadhari:   Kwa vile ugonjwa huu ni wa hatari, watu wabadhirifu, wezi wa mali ya  umma, walaghai, na mafisadi hawawezi kuustahimili. Ugonjwa huu ni kinyume  kabisa na watu hawa hivyo kama hutaki kuambuzizwa hakikisha unaendelea  kujikita katika katika vitendo viovu vya kuharibu mali za umma na  kuivunja vunja nchi huku ukishiriki katika kumegeana hadhina ya  Taifa. Kwa vile ugonjwa huu unaendelea kuambukiza taratibu, kuna  kila dalili hapo
ulipo UNAISHI NA MWATHIRIKA.
Kutoka (Jumanne 04.09.2007): darcity@yahoogroups.com
 
 
 
No comments:
Post a Comment