Thursday, September 27, 2007

“UREMBO SIO UZURI”-HASHIM LUNDENGA

Ni vigumu sana kuzungumzia mashindano ya urembo nchini Tanzania hususani yale ya Miss Tanzania bila kumtaja Hashim Lundenga au Uncle Hashim kama ambavyo wengi hupenda kumuita. Sio tu kwamba Hashim Lundenga ndio aliyafufua tena mashindano ya urembo mwaka 1994 bali kampuni yake ya Lino International Agency Limited ndio haswa mratibu wa mashindano hayo ambayo kila mwaka yanazidi kuwa maarufu na hivyo kuwa tukio linalosubiriwa kila mwaka kwa hamu.

Kwa mwaka huu wa 2007,mashindano ya Miss Tanzania huenda yakawa yameandika historia mpya kabisa nchini Tanzania. Mshindi wa mwaka huu,Richa Adhia, ni mtanzania wa kwanza mwenye asili ya Asia (India) kutwaa taji hilo.Isitoshe ushindi wake umepokelewa kwa hisia tofauti miongoni mwa watanzania jambo ambalo limebakia kuwa gumzo mpaka hivi leo.

Sasa ili kujua kwa undani kuhusu mashindano haya ya urembo huna budi kumuuliza Hashim Lundenga.Hivyo ndivyo tulivyofanya hivi karibuni katika mahojiano naye ambapo aliweka wazi nini kilimsukuma kufufua mashindano haya, anasemaje kuhusu ushindi wa Richa Adhia na nini watanzania tutegemee kutoka katika mashindano ya dunia (Miss World) mwaka huu? Pia Hashim anajibu swali ambalo limekuwa likiulizwa sana na wananchi;Je mashindano ya urembo ni kwa watoto wa “vizito’ peke yao?Haya hapa mahojiano kamili;
(more…)



No comments: