Sunday, November 11, 2007

Oliver Occean mshambuliaji wa Lillistroem (Lillestrøm)
akishangalia goli alilofunga. Picha toka Dagbladet

Timu ya soka ya Lillestroem imekuwa mabingwa wa Kikombe cha soka Norway, baada ya kuifunga timu ya FK Haugesund mabao 2 - 0 kwenye uwanja wa taifa Ullevaal, mjini Oslo. Magoli yote mawili ya Lillestroem yalifungwa na Oliver Occean (Mkanada). Kikombe cha soka Norway huchezwa na timu za ligi kuu pamoja na zile za ligi ya daraja la kwanza.

Uwanja wa taifa, Ullevaal, Oslo.


Zaidi kuhusu ligi ya soka hapa Norway gongola:

http://en.wikipedia.org/wiki/Norwegian_Premier_League



No comments: