Wednesday, May 28, 2008

Mkapa awasha moto


na Salehe Mohamed

UAMUZI wa Rais mstaafu, Benjamin Mkapa kuanza kujibu tuhuma dhidi yake, umeibua malumbano ya hoja kutoka kwa wanasiasa kadhaa ambao wameeleza kushangazwa na majibu na hatua yake hiyo.

Miongoni mwa watu wa kwanza kutoa maoni yao kuhusu kauli hiyo ya Mkapa, ni Mbunge wa Vunjo, Aloyce Kimaro ambaye alikuwa mwanasiasa wa kwanza kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) kumrushia makombora ya tuhuma rais huyo mstaafu, akifanya hivyo ndani ya Bunge.

Akizungumza na Tanzania Daima jana, Kimaro alimtaka Mkapa kujibu tuhuma dhidi yake na kuacha kuwanyoshea kidole wengine kwa matatizo anayokabiliana nayo.


Bofya na endelea kusoma......



No comments: