Friday, May 30, 2008

NASAHA ZA MIHANGWA


Zanzibar:

Uhafidhina,Visasi na

Miafaka isiyodumu (2)



UCHAGUZI wa Januari 1961 uliposhindwa kupata mshindi ilibidi urudiwe Juni 1961 ambapo liliongezwa Jimbo moja la Mtambwe huko Pemba kufanya majimbo ya uchaguzi kuwa 23. Hatua hiyo ililalamikiwa na ASP (kama jinsi CUF ilivyoilalamikia CCM kuongeza majimbo mawili Unguja mwaka 2005) kwamba iliipendelea ngome ya vyama vya ZNP/ZPPP.

Matokeo ya uchaguzi huo uliogubikwa na ghasia yalikuwa kama ifuatavyo:- ZNP/ZPPP viti 13 na ASP viti 10. Hivyo, kwa mara nyingine, matokeo hayo hayakutoa mshindi na machafuko makubwa na ghasia kuzuka ambapo karibu watu 70 waliuawa, zaidi ya 1,000 kujeruhiwa na wengine 1,000 kukamatwa na serikali.


Bofya na endelea kusoma....

No comments: