Sunday, May 25, 2008

Ufunuo mpya:

Ballali aliungama

ukweli kashfa ya EPA



*Majira Jumapili lanasa alichokisema
*Serikali ya Kikwete yasubiri kuumbuka


Na Hassan Abbas


ALIYEKUWA Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Dkt. Daud Ballali, kabla ya kufikwa na mauti yake nchini Marekani, aliungama 'dhambi' yake kuu ya kuhusishwa na kashfa ya ufisadi kwenye Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA), gazeti hili linawathibitishia Watanzania.

Katika ungamo hilo, Ballali (65), aliyekuwa akichukuliwa kuwa mmoja wa watuhumiwa na mashahidi wakuu wanaoweza kueleza nani hasa walikuwa nyuma ya ufisadi huo, imebainika alitaja moja kwa moja mhusika, ungamo ambalo sasa baada ya kifo chake, linaiacha Serikali ya CCM kuwa ndiye mtuhumiwa mkuu.

Kwa mujibu wa nyaraka ambazo gazeti hili limezipata kutoka vyanzo vya kuaminika na maelezo ya siri yaliyotolewa na baadhi ya ndugu zake, Ballali amekufa akiwa ameinyooshea kidole Serikali kuwa ndiyo inayohusika na fedha za EPA zilizochotwa BoT, kauli inayoonesha kuwa yeye alikuwa akipokea tu maagizo ya kuziidhinisha.


Bofya hapa na endelea.......

No comments: