Jakaya Kikwete
agonga mwamba
SASA ni dhahiri kuwa kauli aliyoitoa Rais Jakaya Kikwete kuhusu hadhi ya Zanzibar katika Muungano haijawaridhisha Wazanzibari.
Taarifa kutoka visiwani humo zinaeleza kuwa imeibuka misuguano ya chini kwa chini baina ya viongozi wa serikali visiwani humo na wale wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), yakiibuka makundi miongoni mwao ambao bado hawajaridhika na kile kilichosemwa na Rais Kikwete katika hotuba yake ya kihistoria bungeni wiki iliyopita.
Kwa upande mwingine, msimamo wa Chama cha Wananchi (CUF), ambacho ni chama kikuu cha upinzani visiwani humo, wa kuipinga hotuba ya Kikwete katika kipengele cha hadhi ya Zanzibar, umezidi kuleta mfarakano baina ya viongozi wa CCM na SMZ.
Kilele cha kugonga mwamba kwa kauli ya Kikwete, kilijidhihirisha baada ya maandamano yaliyoandaliwa kuiunga mkono hotuba yake hiyo, na kupata baraka za Jeshi la Polisi juzi, kuvunjwa jana katika mazingira ya kutatanisha.
No comments:
Post a Comment