Tuesday, September 02, 2008

Mzanzibari

aliyekamatwa na

FBI kwa ugaidi

arejeshwa



MTANZANIA aliyekamatwa na makachero wa Marekani kwa kuhusishwa na ugaidi, Suleiman Abdallah Salim (Morris), amerudishwa Zanzibar juzi na Shirika la Msalaba Mwekundu kutoka Afghanistan baada ya kubainika kwamba si gaidi.

Akizungumza na Mwananchi nyumbani kwao maeneo ya Mombasa, Mkoa wa Mjini Magharibi, Zanzibar, huku akionekana mchovu, alisema alikamatwa na makachero wa FBI nchini Somali mwaka 2003 akiwa katika shughuli zake za kibiashara na kuingizwa katika gari bila ya kufahamu anapopelekwa.

Akielezea mkasa uliomkuta akiwa eneo la Abusasu, Mjini Mogadishu alisema baada ya kukamatwa na kuingizwa katika gari hilo huku akipata kipigo kutoka kwa maafisa

hao alisafirishwa hadi Nairobi, Kenya na kutakiwa apeleke mtu wa kumdhamani, lakini aliwaambia kuwa yeye ni Mtanzania na kwamba hana ndugu yeyote jijini humo.


Bofya na endelea>>>>>



No comments: