Mcheza
mpira aanguka na kufariki uwanjani.
Sherehe
za kufurahia uwanja mpya wa mpira wa timu ya Høland, ziliishia kwa masikitiko.
Wapenzi 200 wa timu ya Høland wilayani Nedre Romerike walifika kwenye uwanja
huo mpya wenye nyasi bandia kuangalia mazoezi ya timu hiyo. Mazoezi hayo
yalikuwa ya wachezaji wakongwe waliochezea timu hiyo kwenye miaka ya 80 na 90. Baada ya dakika 20, mchezaji mmoja mwenye
umri wa miaka 40 alianguka kwa kushikwa na ugonjwa wa moyo ghafla na kufariki
hapo hapo uwanjani. Helikopta ilifika hapo haraka na daktari na wahudumu wengine na kujaribu kuokoa maisha ya
mchezaji huyo, lakini ilishindikana.
No comments:
Post a Comment