Thursday, December 01, 2011

leo ni siku ya ukimwi duniani:
tafakari

Leo ni siku ya ukimwi Duniani,

Nimeona nitumie nafasi hii ili tukumbushane na Watanzania wenzangu na hata walio sio watanzania kwani hili ni tatizo kwa kila nchi na kila jamii hapa duniani.

Hili tatizo la ugonjwa huu wa ukimwi (AIDS) limetukabili na inabidi tulichukulie kwa makini na tulipe umuhimu sana kwani limetuathiri sana na linaendelea kutuathiri kuanzia wazee, vijana na hata watoto katika jamii.

Naomba tuwe mstari wa mbele katika kwenda kupima na kujua msimamo wetu na vilevile kuwakumbusha watu wengine kwenda kupima na bila kuogopana.

kwa mfano mtu anapopata mchumba basi asisahau kumkumbusha mwenzake kwenda kupima kwani kufanya hivyo kutaokoa maisha ya wengi hasa ukizingatia wengi wanaoambukizwa katika jamii yetu wameambukizwa na waume au wake zao kwa kuogopa kukumbushana kwenda kupima.

Na baada ya kupima utapata ushauri mzuri toka kwa daktari wako katika jinsi gani ya kujiepusha zaidi hata kama uwe unao ugonjwa au huna.

Katika siku hii ya ukimwi duniani, tumia fursa hii kumkubusha mwenzio kuhusu hili suala hata kama hataki kusikia lakini yatakuwa yamemuingia akilini. 

Naomba kwa mwenye kutaka ushauri zaidi kuhusiana na ugonjwa huu basi awasiliane nami kupitia....... 


Kumbuka sio lazima ujitambulishe kwa jina unaweza kutumia jina lolote ili kuondoa wasiwasi.

-Buhite Aljabry

No comments: