Kwa ajili ya Wahanga wa Mafuriko Tanzania
Habari Jumuiya ya Watanzania Oslo
Nimeguswa sana na suala la mvua na hadha
iliyosababishwa nayo nchini Tanzania, pia nimeguswa na idadi kubwa ya watu
walioachwa bila makazi wala msaada. Nimeangalia ni jinsi gani naweza kuwasaidia
watanzania wenzangu na nimeona ni bora nitume barua pepe hii kwa jumuiya zote
zilizopo nje ya nchi ili kwa pamoja ziweze kuwakutanisha watanzania na
kukusanya chochote kiwezekanacho na kuwepelekea watanzania wenzetu waliopo
Tanzania bila msaada.
Mimi binafsi nipo kusini mwa Ufaransa katika mji
wa Toulouse na kwa bahati mbaya sijapata kujua jumuiya wa Watanzania katika mji
huu wala Paris na pia sijabahatika kukutana na mtanzania mwingine zaidi ya
mmoja ambaye tupo nae pamoja chuo.
Asanteni na natumai wote tutashikama kwa ajili ya
nchi yetu Tanzania.
Mponda Malozo
+33 684 21 45 01
+33 684 21 45 01
Toulouse, France
Skype: Malozo.
Web: www.unawetanzania.org
Web: www.unawetanzania.org
No comments:
Post a Comment