TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Bibi Amina Saidi Mrisho kuwa Kamishna wa Sensa ya Mwaka 2012.
Aidha,
Rais Kikwete amemteua Bibi Seraphia R. Mgembe kuwa Mratibu wa Mpango wa
Kurasimisha Raslimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA).
Taarifa
iliyotolewa na kutiwa saini Dar es Salaam leo, Jumanne, Februari 21, 2012, na
Kaimu Katibu Kiongozi, Bwana Peniel Lyimo imesema kuwa uteuzi huo umeanza jana,
Februari 20, mwaka huu, 2012.
Taarifa
ya Bwana Lyimo imesema kuwa kabla ya uteuzi wake, Bibi Amina Mrisho alikuwa
Mkuu wa Mkoa wa Pwani.
Katika
taarifa tofauti iliyotolewa na kutiwa saini pia mjini Dar es Salaam leo, Jumanne,
Februari 21, 2012, na Katibu Mkuu Ikulu, Bwana Peter Ilomo, imesema kuwa uteuzi
huo wa Bibi Mgembe umeanza pia jana, Jumatatu, Februari 20, 2012.
Bwana
Ilomo amesema katika taarifa yake kuwa kabla ya uteuzi wake Bibi Mgembe alikuwa
Mkurugenzi wa Utawala na Fedha wa MKURABITA.
Bibi
Mgembe anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bwana Ladislaus Salema ambaye
amestaafu kwa mujibu wa sheria.
Mwisho.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
21 Februari, 2012
No comments:
Post a Comment