Sunday, March 04, 2012

Msiba Stockholm, Sweden



Tanzania University Sports Association - TUSA, Wana Michezo jamaa na marafiki
.
Tumepokea taarifa ya kifo cha mpendwa wetu Ndg. Andrea Lesso Hange ambaye hadi kifo chake alikuwa Katibu Mkuu Msaidizi wa TUSA na Mhadhiri Msaidizi wa UDSM. Kifo chake  Kimetokea tarehe 02/03/2012 huko Stockholm, Sweden alikokuwa masomoni. Taarifa kamili za kifo chake na taratibu zingine zinasubiriwa kutolewa rasmi na uongozi wa chuo. Zitakapokuwa tayari mtajulishwa kinachoendelelea. Kwa hivi sasa Msiba upo nyumbani kwake Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Karibu na Hall One. Tunawaomba watu wote tushirikiane katika kipindi hiki kigumu. Pia tunaomba kama TUSA na marafiki zake tutoe rambirambi zetu kupitia namba zifuatazo,

1. TIGO Pesa - 0713263556
2. Voda Pesa - 0765694533
3. Airtel Money - 0786027666

Pia unaombwa kutembelea Blog ya TUSA


kwa kupata taarifa nyinginezo kuhusu msiba huu.


Asante sana kwa ushiriakiano wenu

NOEL KIUNSI
KATIBU MKUU TUSA
 
NOEL B. KIUNSI
PRINCIPAL GAMES TUTOR
UNIVERSITY OF DAR ES SALAAM
P.O. BOX 35091
DAR ES SALAAM
TANZANIA

 +255713263556      
  

No comments: