Wednesday, April 04, 2012


Aspirini inaweza kuzuia saratani

Kumeza kidonge cha aspirini kila siku inaweza kuzuia na hata kutibu saratani. Taraifa hii ni kwa mujibu wa utafiti mpya. Matokeo ya utafiti huo yalichapishwa na jarida la matibabu la The Lancet, na hivyo kuzidisha kuonyesha manufaa ya aspirini katika matibabu ya saratani.

Watu wengi tayari wanatumia Aspirini kama dawa ya maradhi ya moyo. Lakini wataalamu wanaonya kuwa hakuna ushahidi wa kutosha kuelezea watu kutumia aspirin ili kuzuia saratani na hata vifo vinavyotokana na saratani.

Wataalamu hao wanaonya kuwa dawa hiyo inaweza kusababisha athari kubwa kama kuvuja damu tumboni.

Prof Peter Rothwell,wa chuo kikuu cha Oxford akiwa na wakufunzi wengine ambao wamefanya utafiti wa hivi karibuni, tayari walikuwa wamehusisha aspirin na kuzuia aina ya saratani hasa saratani ya matumbo.

Vidonge vya Asprin
Lakini utafiti wao wa awali, ulipendekeza kuwa watu wanahitaji kutumia dawa hiyo kwa takriban miaka 10 ili iweze kufanya kazi hiyo.

Sasa wataalamu wanaamini kuwa uwezo wa dawa hiyo kuzuia saratani, hutokea mapema mno kati ya miaka mitatu na mitano. Hii ni kwa mujibu wa taarifa mpya kutoka kwa majaribio 51 yaliyohusisha wagonjwa 77,000.

Lakini wakati kikundi cha wataalamu, kilichoongozwa na Profesa Rothwel kilidurusu wangapi kati ya watu waliohusika katika utafiti huo walipata kuugua saratani na hata kufariki kutokana na ugonjwa huo, waligundua kuwa vifo vilitokana pia na matumizi ya aspirin.


Kuzuia kusambaa kwa Saratani
Kwa mtu anayetumia kiwango kidogo cha dawa hiyo kila siku, ilionekana kupunguza idadi ya visa vya saratani kwa robo baada ya miaka mitatu pekee.

Ni watu tisa waliogungulika kuwa na saratani katika watu elfu moja kila mwaka ikilinganishwa na watu kumi na mbili kwa watu elfu moja kwa wale waliomeza tembe hizo.

Pia ilipunguza idadi ya vifo vilivyookana na saratani kwa asilimia kumi na tano.

ONYO - USITUMIE DAWA BILA USHAURI WA DAKTARI TAFADHALI  SANA .

Habari hii kutoka BBC Kiswahili

No comments: