Saturday, April 14, 2012





TAFAKARI...! CHUKUA HATUA!!
Hivi tunawezaje kuishi kwa matumizi yafuatayo kila mwezi?

  1. Matumizi nyumbani;
  2. Chakula,
  3. Umeme,
  4. Gesi,
  5. Maji,
  6.  Soda/juisi za wageni
  7.  Ada za watoto zinazolingana na za chuo kikuu
  8. Matibabu hospitalini,
  9.  pesa ya walinzi kwa mwezi,
  10. sherehe za kuaga na kukaribisha mwaka mpya,
  11. Zaka ya kanisani na misikitini
  12. Kupanda Mbegu/ Sadaka Shukurani ya Neno
  13. Tozo za flying (wazoa taka wa mikokoteni ambao huzitupa hapo hapo)
  14. Madalali wa nyumba/viwanja
  15.  Pango la nyumba
  16.  Fremu ya biashara/ofisi
  17. Mazakayo wa mitandao ya simu [airtime vouchers]
  18.  Mafuta ya gari
  19. Walinda/waosha magari (oya sista/blaza, mdogo wako nipo apaaa)
  20. Tozo za kuegesha magari
  21. Makato ya Mikopo
  22.   Tozo za internet cafe ili uweze ku-surf
  23.  Rambirambi ya mfiwa mtaani au ndugu
  24. Michango ya harusi/send off/kitchen party ya ndugu au rafiki
  25.  Zawadi ya harusi/ sendoff/kitchen party
  26. zawadi ya kumuaga mfanyakazi mwenzenu
  27. zawadi michango ya komunio ya 1 & 2 na kipaimara na birthday
  28. Michango ya birthday party na zawadi ndugu wa kule kijijini
  29. Mshahara wa Hausigeli na na hausiboi
  30.  Bodaboda,
  31. teksi na bajaj
  32.  Duka la dawa
  33.  Tuisheni ya mtoto
  34.  Kuchangia wahanga wa mabomu, mafuriko na vistula.
  35.  Kwenda kumuona mtoto aliyezaliwa,
  36.  Kununua CD/DVD ya Uzinduzi wa Kwaya yetu
  37. Chakula cha mbwa
  38. Machango wa Ujenzi wa Kupanua Kanisa
  39.  Kuchangia Uinjilisti Masasi /DRC
  40. Auting ya kitimoto
  41.  Ujenzi wa Nyumba Mwabepande
  42.  Kuendeleza shamba mkuranga (linalotaka kutaifishwa kwa kutoendelezwa)
  43. Kwa wale wenzetu wanaokwenda umbali wa Viti Virefu, moja moto moja baridi
  44. Maji ya Traffik
  45.  Chai ya Nesi na Daktari,
  46. Kahawa ya Hakimu, Karani na PP
  47. Vishoka waunganisha maji na umeme
  48. Kidogodogo cha mjumbe na mtendaji wa mtaa
  49. Mia mbili ya watoto wa mtaani/ombaomba,
  50. kitu kidogo cha wale wanaolazimisha kuosha kioo cha gari kwenye foleni.
  51.  umeme na gesi vilivyopanda bei,
  52. maji yaliyoadimika,
  53. bado contingency maana huu usafiri unaotembelea ball joint,bush,fen belt havijafa...bado service,
  54. bado msosi wa mchana kazini esp kama maofisi yetu mama ntilie wanakaribiana bei na restaurants  
  55. sare,baby show...
  56. bado hujatoa watoto outing jumapili n.k
  57. Kutunza wazazi/Wakwe
  58. Kuchangia ujenzi wa barabara/zahanati nyumbani utokako na mjini uishipo nk....nk


Hapo mwajiri amekuongezea mshahara kwa 7% tu wakati inflation ni above 19%. Ndipo unapoimba "...Mwokozi nitoe roho niepuke hili balaaa..."

Ukifikiria kwa makini unajiuliza watanzania wanasurvive vipi kwa style hii??? 

Imeletwa kwenye blogu toka Tanzanet (www.tanzanet.org)

No comments: