Monday, July 30, 2012

Mauaji ya balozi yachunguzwa Kenya


Marehemu Olga Fonseca


Polisi wa Kenya wanasema kuwa wanaendelea na uchunguzi, juu ya mauaji ya balozi mpya wa Venezuela nchini humo, ambaye aliuwawa Ijumaa.

Olga Fonseca, aliyeanza kazi Kenya kati ya mwezi Julai, alikutiakana ameuwawa nyumbani kwake, na watu sita wamekamatwa hadi sasa.

Watu hao sita wamekamatwa siku mbili tu baada ya balozi huyo kupatikana amefariki nyumbani kwake.

Siku ya Ijumaa, polisi walisema kuwa maiti ya Bi Olga Fonseca ilipatikana kitandani mwake lakini sababu za kuuwawa kwake hadi sasa hazijulikani.
Bila ya kutoa maelezo zaidi, polisi wamesema kuwa wanawashikilia watu sita kuhusiana na kifo cha balozi huyo.

Taarifa kutoka wizara ya maswala ya njee ya Kenya imesema kuwa wafanyikazi katika makaazi ya balozi huyo waliwasilisha malalamiko yao kwa polisi baada ya kufutwa kazi hivi majuzi.

Inadaiwa kuwa bi Fonseca aliwafuta kazi baada ya wao kukataa kuondoa malalamiko kuhusu madai ya kunyanyaswa kijinisia na mtangulizi wa balozi huo.
Hata hivyo polisi wamesema wanachunguza madai hyao.

Chanzo: BBC Kiswahili

No comments: