Sunday, January 27, 2013



Na Haruni Sanchawa

MWANAMKE mmoja, Esther Meshaki amelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili tangu Januari 18, 2012 hadi leo na hajawahi kutembelewa na ndugu yake au rafiki yeyote, Uwazi limegundua.

Afisa Habari wa Hospitali ya Muhimbili, Aminiel Aligaesha alisema wiki iliyopita kuwa mgonjwa huyo aliletwa na polisi waliodai kumuokota barabarani katika eneo la Temeke akiwa hajitambui. 

“Wataalamu wetu wamejitahidi kutoa huduma kwa mgonjwa huyu kufikia kiwango cha kuweza kuongea mwenyewe na kujitambua vizuri.

“ Changamoto tuliyonayo ni kuwa mgonjwa huyu tangu alazwe hakuna ndugu wala jamaa yake yeyote aliyejitokeza. Hivyo kwa sasa tunatafuta ndugu wa mgonjwa huyu ambaye amepata nafuu ili aweze kujiunga na familia yake,” alisema Aligaesha.

Alifafanua kuwa katika kufanya udadisi imegundulika kuwa Esther alizaliwa Kigoma vijijini katika Kijiji cha Kigogwe mwaka 1985. Kabila lake ni Muha na anasema mama yake anaitwa Dotto Alfred na baba yake anaitwa Meshaki Alfred ambao hata hivyo, walitengana.

“Ndugu, jamaa au yeyote mwenye taarifa za mgonjwa huyu naomba awasiliane na Ofisi ya Uhusiano Hospitali ya Muhimbili kupitia namba 0755 648 636,” alisema afisa habari huyo.

No comments: