Sunday, February 17, 2013

Padri Evarist apigwa risasi na kuuawa Zanzibar


Paroko wa Kanisa la Katoliki Minara Miwili Zanzibar, Evarist Mushi amefariki dunia baada ya kupigwa risasi saa 1.00 asubuhi na kufariki kabla hajafika hospitali ya Mnazi Mmoja. Paroko huyu amepigwa risasi akishuka katika gari lake wakati akienda kuendesha ibada ya saa 3.00 leo.

Padri Evarist Mushi amepigwa risasi kichwani na kufa papohapo na watu wasiojulikana akiwa njiani anaenda kuendesha misa katika Kanisa la Mt.Theresia eneo la Mtoni Zanzibar.

Msemaji wa Jeshi Polisi Zanzibar Inspekta Mohamed Mhina amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na amesema kuwa padre huyo ameuawa wakati akijiandaa kuingia kanisani akitokea kwenye gari yake ambapo ndipo alipofikwa na umauti huo.

Jeshi la Polisi visiwani humo kupitia kwa Msemaji wake Mkaguzi wa Polisi, Mohamed Mhina limelaani mauaji hayo na na kusisitiza kuwa Jeshi limeanza msako mkali wa kuwabaini wauaji hao.

Hili ni tukio la pili kutokea Zanzibar ambapo tukio la kwanza lilitokea kwa Padre Ambrose Mkenda kupigwa risasi na kujeruhiwa na watu wasiojulikana.


No comments: