Mwanasiasa mkongwe Mzee Kingunge Ngombale Mwiru akisisitiza jambo wakati uzinduzi wa kitabu historia ya Hayati Sheikh Kaluta Amri Abedi katika hafla iliyofanyika leo kwenye ukumbi wa Karimjee jijini Dares Salaam.Kushoto ni Balozi Mstaafu Job Lusinde na kulia ni Brigedia Hashimu Mbita.
Na Frank Shija na
Benedict Liwenga - Maelezo
VIONGOZI wahimizwa MWANASIASA mkongwe Mzee Kingunge
Ngombale Mwiru kuwataka viongozi nchini kukienzi na kuthamini lugha ya
Kiswahili ili kuendelea kujenga taifa lenye umoja na mshikamano.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Mzee Kingunge ambaye
alikuwa mgeni ramsi katika hafla ya uzinduzi wa Kitabu cha Historia
ya Hayati Sheikh Kaluta Amri Abedi iliyofanyika kwenye ukumbi wa
Karimjee, jijini Dar es Salaam .
“Hatima ya Taifa inategemea lugha ya Kiswahili.
Viongozi wanawajibu mkubwa katika kuhakikisha kuwa lugha ya Kiswahili inakuwa
kwani wao ndio wanaweza kukipandisha au kuiua lugha ya Kiswahili kwakuwa jamii
inawategemea kwa kiasi kikubwa,” alisema Mzee Kingunge.
Aidha Mzee Kingunge anawaasa kuwa
wazalendo na kutumia lugha ya hiyo kwa ufasaha tofauti na ilivyo sasa katika
shughuli mbalimbali mfano Bungeni.
Hata hivyo, aliunga mkono lugha hiyo
kuwa rasmi kufundishia, lakini ametoa changamoto kuwa yatupasa kuwa makini
katika kuitumia hususani katika ngazi elimu ya msingi, sekondari hadi vyuo
vikuu.
Mzee Kingunge alitolea mfano wa wajukuu zake kuwa
masomo mengine kama vile hesabati wanapata alama 90 hadi 95,lakini
lugha hiyo wanapata alama ya 60 mpaka 70. Hivyo inaelekea ufundishaji wake ni
tatizo.
“Kama kufundisha lugha ya Kiswahili katika elimu ya
sekondari ni tatizo na Kiingereza ni tatizo . Kiswahili kipi kifundishwe katika
elimu ya Chuo Kikuu,”alisema. Huku akitolea mfano kuwa kumekuwa na matumizi ya
maneno ambayo si sahihi kama vile neno masaa badala ya saa.
Kwa upande wake mwanazuoni na mdau wa lugha
hiyo Profesa Mugyabuso Mulokozi na Profesa Joshua
Madumula wameiomba serikali kuwa na utaratibu wa kuenzi fasihi
za Watanzania.
No comments:
Post a Comment