YAH:
UTARATIBU MPYA WA KULIPIA
ADA YA VISA YA KWENDA TANZANIA
Kwa
wana-diaspora wanaohitaji Visa ya Tanzania,
Tunapenda
kuwaarifu kuwa kuanzia tarehe 1 Mei 2013, Ubalozi haupokei fedha taslimu wala
“Credit Card” kwa malipo ya visa.
Malipo
yote sasa yanafanyika kwenye akaunti yetu ya Benki ya NORDEA
Plus Giro Na. 103 7471-8 kwa walipaji walioko Sweden. Wanaolipia nje
ya Sweden watumie (BIC/Swift Address: NDEASESS na IBAN:
SE2895000099604210374718 (bila kuacha nafasi).
Risiti ya
malipo iambatanishwe na fomu ya maombi utakapotuma maombi kwa posta au
utakapoleta maombi kwa mkono Ubalozini.
Tafadhali
tunaomba ujiepushe na usumbufu kwako kwa kulipia ada
ya visa Benki kabla ya kuleta maombi yako Ubalozini.
Taarifa
hii ipo kwenye tovuti ya Ubalozi tangu mapema mwezi Aprili kupitia “link”
ifuatayo: http://www.tanemb.se//index.php?option=com_content&task=view&id=178&Itemid=36
Unakaribishwa
pia kuwasiliana na Ubalozi kwa njia ya simu au barua pepe endapo utahitaji
maelezo ya ziada.
Tunawaomba
na tunawashauri muendelee kutembelea mara kwa mara tovuti ya Ubalozi, www.tanemb.se ili
kupata habari na taarifa mbali mbali kutoka Ubalozini.
Tunatanguliza shukrani zetu
Jacob Msekwa
KNY: BALOZI
No comments:
Post a Comment