Inapohusu utamaduni wa kucheza ngoma na dansi:
Ngoma nyingi za baadhi ya makabila ya Tanzania, zina miondoko ya kinamna hiyo. Ngoma za makabila mengi ya kusini na ya pwani, miondoko kama inavyoonyesha hapo chini ni ya kawaida. Ngoma kama Sindimba, Sikinde, Msondo na kadhalika. Jinsi gani miondoko hii inavyochukuliwa na tamaduni za kizazi kipya ndio suala kubwa hapa. Kufuru inayozungumziwa hapa ni jinsi gani inavyochezwa na wapi inaonyeshwa kwenye hiki kizazi kipya! Habari hizo hapo chini kutoka: Global Publishers Tanzania.

Shabiki mmoja ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja, katikati ya wiki iliyopita alifanya kufuru tupu katika ukumbi wa DDC Kariakoo, jijini Dar es Salaam baada ya kunengua kwa staili za ajabu na kuwaacha hoi watu waliomshuhudia....

Ilikuwa kama mchezo wa kuigiza kwani baada ya muziki kukolea, dada huyo aliyekuwa 'ameunasa' mtungi vilivyo alinyanyuka alipokuwa amekaa na kupanda jukwaani kwa kasi, kisha kuanza kukata mauno kwa ustadi mkubwa na kuwafanya wapenzi wa kundi hilo kuduwaa.

Hata hivyo, baada ya kumaliza kufanya mambo yake jukwaani dada huyo alijikuta akijuta, baada vijana wa kihuni kumvamia na kumtaka kuondoka naye kusikojulikana.
Kama si juhudi za mabaunsa wa kundi hilo, wakishirikiana na wale wa ukumbi huo, dada huyo angechukuliwa na vijana hao na kufanyiwa kitu mbaya.
No comments:
Post a Comment