Thursday, July 23, 2009

Tahadhari toka kwa

afande Kova




Tafadhali wajulishe wote wanaohusika kwamba kuna kundi kubwa la majambazi wenye silaha kali, ambao wameingia Jijini Dar es salaam hivi karibuni. Wahalifu hao ni pamoja na Wakenya ambao wana tabia ya kupora fedha katika taasisi kubwa kama, mabenk, kampuni za mafuta na sehemu zenye biashara kubwa n.k .

Aidha watu hawa wana mbinu ya kula njama na watumishi wasiokuwa waaminifu. Ni muhimu mkafuatilia mienendo mbalimbali katika benk zenu na sehemu zilizotajwa hapo juu pamoja na kuimarisha usalama julisheni kwa message kupitia namba

0783034224

au kwa simu ya mdomo

0754-034224

0787034224

zote ni namba za Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Polisi Dar es salaam.

Namba zingine za simu ni

0754- 276217

0776880000

namba hizi ni za mkuu wa Upelelezi Kanda maalum.

Lengo la maelezo si vitisho kwenu bali ni tahadhari muhimu , inayofaa kuzingatiwa,

S. H. Kova - SACP
KAMANDA WA KANDA MAALUM

DAR ES SALAAM


No comments: