Saturday, November 24, 2007

Bi. Fatma Karume.


TAARIFA KWA UMMA

Sisi Chama cha wanasheria Tanzania Bara tumepokea kwa masikitiko nakala ya barua kutoka kwa Hakimu mkazi wa Mahakama ya Kisutu Mh. Addy Lyamuya kwenda kwa Hakimu Mkuu Mfawidhi wa Mahakama ya Kisutu kuhusu malalamiko dhidi ya Wakili Msomi wa kujitegemea Fatma Karume kwenye shauri la ndoa kati ya Bwana Sadiq Ahmed Walji (Petitioner) na Bibi Saeeda Hassan (Respondent) leo tarehe 22/11/2007.

Barua hii ilieleza malalamiko dhidi ya Wakili Msomi Fatma Karume ambaye ni mwanachama wa chama cha Wanasheria Tanzania Bara ambaye anatuhumiwa kusumbua mahakama na kuchelewesha kesi kwa vurugu ambazo hazikuwa za lazima tarehe 21/11/2007 katika mahakama ya Kisutu wakati shughuli za mahakama zinaendelea.

Tumeijibu barua ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu na kumhimiza Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama wa Kisutu, Mheshimiwa Mwangesi, ayasikilize malalamiko haya ili kuthibitisha ukweli wa tukio hilo kwa haraka. Sisi kama Chama wa Wanasheria tuna wajibu wa kutetea wanachama wetu pale wanapoonewa na pia tuna wajibu wa kuwachukulia hatua kuendana na sheria na kanuni zetu pale inapothibitika kwamba mwenendo wao umekiuka maadili ya taaluma yetu.

Tuko tayari kushirikiana na Mahakama kufikia maamuzi ya kweli na haki. Endapo itathibitika kwamba Wakili Msomi Fatma Karume aliyafanya hayo yanayodaiwa itakuwa ni kitendo ambacho kitastahili kukemewa/kukaripiwa na kutolewa adhabu kwa mujibu wa kanuni za sheria kwa sababu ni kinyume na maadili ya Mawakili ambao wana majukumu kama maafisa wa Mahakama kulinda uhuru, kuiheshimu na kuisaidia Mahakama kufikia maamuzi huru na haki.


Joaquine De-Mello
Rais,
Tanganyika Law Society
22 Novemba 2007

Kutoka kwa Maggid Mjengwa.



2 comments:

Anonymous said...

Mahakimu wa Mahakama hiyo inaonekana wanchukua rushwa na wanaharibu kesi nyingi.

Maoni yangu ni kwamba kwasababu hakimu wa kwanza alipelekwa Takukuru na wengine wantaka kumkomoa Karume lakini wanamkomoa mtoto wa miaka miwili.

TUPAMBANE NA RUSHWA!

endelea tuu dada...HONGERA!

Anonymous said...

Tatizo sisi watanzania tumezoea sana mteremko, ata rushwa ni vile vile kama ugali wa kila siku tu. Ukishikwa na askari, si kwa ajili ya makosa kwenye gari yako lakini ni njaa zake tuu, vile vile system yote hapo tanzania. Hii kesi ni sawasawa na ukiwa na askari wa kulinda nyumbani, ungependa huyo askari alinde nyumba yako na ulale kwa usalama au askari mpumbavu anaye lala tu na akipewa hela na wezi aanze kuwa saidia wezi namna ya kuvunja nyumba yako. Huyo dada Fatma ndiyo kiboko yao, Fatma wachape viboko hawa sawasawa na tuwaondoe ugonjwa wa cancer mahakamani.