Friday, November 23, 2007

Mwanafunzi afanyiwa umafia!

Mwanafunzi wa kidato cha tatu (jina lake na shule anayosoma kapuni) hivi karibuni amejikuta akifanyiwa umafia na wanaume wanne anaodaiwa kuwagonganisha kimapenzi.

Habari kutoka wilayani humu mkoani Shinyanga zilisema kuwa, binti huyo ambaye pia amedaiwa kuwa muimba kwaya mzuri alijikuta akifanyiwa vitendo vichafu kwa zamu na vijana wasiojulikana.

Ilidaiwa kuwa, kabla ya kufanyiwa umafia huo mwanafunzi huyo alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na miongoni mwa vijana hao kwa nyakati tofauti....

“Tamaa ya chipsi kuku ndiyo iliyomponza, vijana hao wote alikuwa anafanya nao mapenzi, huenda siku hiyo waliamua kumkomesha kwa tabia hiyo ya kuwagonganisha,” kilisema chanzo chetu ambacho kilidai kufahamu nyendo za mwanafunzi huyo.

Ilidaiwa kuwa siku ya tukio msichana huyo na mmoja kati ya wapenzi wake walipanga ahadi ya kukutana kwenye gesti bubu (isiyo rasmi), ilioyoko eneo la Nyihogo ambako vijana wengine watatu walikwenda pia.

Habari zilisema wakati msichana huyo akiwa chumbani na mvulana aliyepanga kukutana naye, vijana hao waliingia na kuanza kubadilishana kwa staili ya mtu kutoka na mwingine kuingia kiaina.

Hata hivyo, licha ya binti huyo kukutwa na wahudumu akiwa hoi alisita kuripoti tukio hilo kituo cha polisi kwa madai kuwa atajiaibisha.

Uchunguzi uliofanywa na Amani ulibaini kuwa, wasichana wengi katika maeneo ya miji wamekuwa wakirubuniwa kwa vitu vidogo na kujikuta wakifanyiwa vitendo hivyo viovu.

Gazeti hili linawaomba mabinti kuwa makini na mfumo wao wa maisha na kuhakikisha wanaangalia masomo kwanza na kuweka mapenzi pembeni.

No comments: