Sunday, November 25, 2007

Tovuti ya JWTZ Yazinduliwa...

Kwa mara ya kwanza, jeshi la wananchi la Tanzania(JWTZ) limezindua tovuti yake yenye lengo la kuongeza Ushirikiano kati yao na wananchi. Tovuti hiyo ni www.tpdf.go.tz iliyoznduliwa rasmi jana jijini Dar es Salaam na Mnadhimu mkuu wa jeshi hilo,Luteni Jenerali Abdulrahaman Shimbo pichani, kwenye bwalo la maofisa wa jeshi hilo Upanga, Dar es salaam.

Luteni Jenerali Abdulrahaman Shimbo alisema lengo la tovuti hiyo ni ukuaji wa sayansi na teknolojia hali inayofanya dunia kuwa kijiji kutokana na ukweli kwamba sekta ya mawasilianano kupanuka, '' JWTZ lliona si vyema kuendelea kufunga funga mambo yetu na kuwa wapweke na tunaamini tovuti yetu ni endelevu, tunawaomba wananchi kutembelea tovuti hii na kutoa maoni yao kuhusu utendaji wetu na kutushauri. tupo tyari kuyapokea na kuyafanyia kazi yote mtajayotushauri kwa lengo la kuboresha jeshi jeshi,'' alisema Luteni Jenerali Shimbo.

Unaweza kupata habari nyingi juu ya jeshi letu la JWTZ kwa kutembelea WWW.TPDF.GO.TZ

Kutoka: http://haki-hakingowi.blogspot.com


No comments: