Saturday, December 22, 2007


Kohinoor Nordberg. Picha na Ny Tid


Mnorwejiani wa mwaka 2007


Jarida la Kinorweji "Ny Tid" limemtaja mwanadada Kohinoor Nordberg (34), kuwa Mnorweji wa mwaka 2007. Kohinoor alijulikana baada ya mumewe, Ali Mohammed Farah (37) kupigwa bila makosa na kuumizwa vibaya kwenye bustani ya Sofienberg , jijini Oslo, Agosti 6, mwaka huu. Baada ya Ali kuumizwa gari la wagonjwa na wahudumu wake lilikuja na gari la polisi la polisi lilikuja na kumwanglia Ali.


Kohinoor akipongezwa kwa kuwa Mnorweji wa mwaka 2007

Polisi walimwambia Ali kuwa anadanganya hakuumia kama ilivyokuwa inaonyesha. Licha ya watu wengi waliokuwepo kama mashahidi kutoa maelezo ya kuumizwa kwa Ali. Wahudumu wa gari la wagonjwa walimwacha Ali kama alivyo. Ilibidi Kohinoor na wengine waliokuwepo, wamchukue Ali kwenye Taxi hadi hospitali dharura "Ermegency room - ER" hapo napo ilichukua masaa mawili kabla ya Ali kupelekwa hospitali ya Ullevaal.

Tukio hilo lilileta mtafaruku wa aina yake. Polisi na wahudumu wa gari la wagonjwa waliandika ripoti za uongo. Kitu ambacho kilisaidia ni kuwa kulikuwa na watu wengi waliorekodi tukio hilo.


No comments: