Friday, May 23, 2008

Kwa nini Pinda ni kipenzi

kwa Kikwete kuliko Dr Shein


Na Stanislaus Kirobo

Tangu ateuliwe kushika wadhifa wa Uwaziri Mkuu takriban miezi mitatu iluiyopita, Mizengo Pinda amemwakilisha Rais Jakaya Kikwete katika shughuli za nje ya nchi mara tatu. Kwa wastani amefanya hivyo mara moja kila mwezi.

Katikati ya mwezi wa nne (tarehe 17 Aprili) Waziri Mkuu Pinda alimwakilisha Rais mjini Nairobi wakati wa kuapishwa kwa baraza jipya la mawaziri wa serikali shirikishi iliyoundwa.

Mapema mwezi huu Pinda alimwakilisha Rais huko Maputo, Mozambique, kwenye mkutano wa Nane wa Muungano wa maendeleo ya Elimu barani Afrika (ADEA). Na mapema wiki hii Pinda alimwakilisha Rais katika mkutano wa siku tatu wa Jukwaa la Uchumi wa Dunia (World Economic Forum) kuhusu Mashariki ya Kati.


Bofya na endelea kusoma....


No comments: