Monday, May 26, 2008

Mbowe atoa kauli nzito

kifo cha Ballali


na Lucy Ngowi


MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe amesema kifo cha aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu (BoT), Daudi Ballali kina mkono wa baadhi ya vigogo wa serikali, kwa sababu alikuwa shahidi muhimu katika vita ya ufisadi.

Mbowe ambaye anakuwa kiongozi wa kwanza kutoa kauli hiyo nzito, alisema hayo wakati alipokuwa akizungumza na wakazi wa Mtaa wa Ufipa, pamoja na waandishi wa habari katika Makao Makuu ya chama hicho, Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Alisema kuna kitendawili kinachotegwa sasa na baadhi ya vigogo wa Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kwa kuwa Ballali alikuwa shahidi muhimu sana katika vita ya ufisadi aliyodai kufanywa na chama tawala.

Mbowe alisema, tangu Ballali alipoondoka nchini Agosti, mwaka jana, vyombo vyote vya habari viliandika vikidai gavana huyo wa zamani ana ushahidi wa kina kuhusu ubadhirifu wa pesa za BoT, matokeo yake Rais Jakaya Kikwete alitengua uteuzi wake na kuunda kamati ya kuchunguza ufisadi huo.

Mwenyekiti huyo wa CHADEMA alisisitiza kuwa, Ballali hakula peke yake, bali alikula na baadhi ya viongozi waandamizi wa serikali ya awamu ya tatu na ya nne na kuongeza kuwa, hata baadhi ya fedha zilizotumika wakati wa kampeni ya mgombea wa CCM, zilitokana na fedha za EPA.


Bofya na endelea kusoma....


No comments: