Thursday, May 01, 2008






Msanii wa hiphop Mwanafalsafa aka Mwana FA ametoka na
tovuti mpya iitwayo http://www.binamu13.com

Katika tovuti hiyo wasomaji wanaweza kujipatia taarifa mbalimbali zinazomhusu yeye kama historia yake, nyimbo zake, albam na picha zake, nguo zake na kadhalika.

Mwana Fa aliyezaliwa miaka 27 iliyopita jijini Tanga, alianza kujishughulisha na mambo ya muziki mwaka 1993 wakati huo akiwa shule ya msingi jijini Tanga.

Mwana Fa alianzisha kundi lake lijulikanalo kama Black Skin akiwa na wanafunzi wenzake Robilus na Getheerics mwaka 1995. Mwaka 1998 aliingia jijini Dar es Salaam kwa ajili ya masomo ya juu katika Sekondari ya Ununio Islamic High School, akiwa anachukua masomo ya Physics, Chemistry na Mathematics.

Baada ya kuhitimu mwaka 2000, alijiingiza katika mambo ya muziki ambapo mwaka 2003, alipata tuzo za Kili kwa kuwa mwanamuziki bora wa hip hop na wimbo wake ‘Alikufa Kwa Ngoma’. Vilevile mwaka 2006 albam yake ya Unanitega ilipata tuzo ya Kili katika kitengo cha albam bora ya hiphop. Albam zake alizokwishatoa ni kama ‘Mwanafalsafani’, ‘Toleo lijalo’ na 'Unanitega'. Baadhi ya nyimbo zinazowika sasa hivi ni 'Asubuhi' na 'Nangoja Ageuke' akiwa ameshirikiana na AY, nyimbo ambazo utakuta kwenye albam yao ya 'Habari Ndio Hiyo' waliyoitoa mwaka jana.

Ukiachana na muziki Mwana FA anauza pamba zake zinazokwenda kwa jina a 'Binamu' na hutoa msaada kwa wasiojiweza kupitia shirika la Sawa Sawa Foundation.


Kind Regards,
255 Enterprise Inc
Email: info@2five5.com
Website:www.2five5.com
Mobile: +44 7722 322 992



No comments: