Thursday, May 01, 2008


Vibwanga Vya Tabata


Wakazi wa maeneo ya Tabata jijini Dar es Salaam,wakichungulia ndani ya gari kumuangalia msichana Rehema Kefa (18) anayedaiwa kuwa ni mchawi baada ya kukamatwa akiwa katika Zahanati akidai kutafuta mtoto na damu ya kunywa.




Ofisa wa ngazi ya juu kutoka jeshi la Polisi akimhoji Msichana Rehema Kefa (18)kwenye kituo cha Polisi cha Buguruni jijini Dar es Salaam baada ya Msichana huyo kukamatwa akiwa katika Zahanati moja iliyoko Tabata akiwa katika harakati za kutafuta mtoto kwa nia ya kunywa damu yake.Lakini Msichana Rehema alipokuwa anajieleza baada ya kufikishwa katika kituo hicho cha Polisi Buguruni,jijini Dar es Salaam leo alidai yeye ni mkazi wa Tabata Msimbazi na kukiri kuwa alifika katika Kituo cha Afya Tabata kwa agizo la bibi yake.Picha zote kwa Msaada wa Mpiga Picha Maalum wa TSN na Mdau Mpoki Bukuku.




Mchawi Mwingine abambwa
Tabata..


Mkazi wa jijini Dar es Salaam, Rehema Kefa (18) akiwasilisi katika Kituo cha Polisi Buguruni jijini Dar es Salaam,baada ya kukamatwa akiwa katika Zahanati moja iliyoko Tabata akiwa katika harakati za kutafuta mtoto na kunywa damu yake.Msichana huyo,alikamatwa na kuwekwa chini ya uangalizi wa polisi,baada ya kukiri kuwa ameanza kufanya kazi zinazodaiwa kuwa ni za kichawi akiwa na miaka mitano.

----------------------------------------------------------------
Siku tatu tu baada ya kijana kukamatwa na kichwa cha mtoto, kijana mwingine, safari hii msichana, amekamatwa katika hospitali ya Tabata iliyopo Wilaya ya Kinondoni jijini Dar kwa tuhuma za kutaka kuiba mtoto wodini.

Rehema Kefa(18) Mkazi wa Mkuranga alikutwa akitaka kumtorosha mtoto huyo leo aliyekuwa katika wodi ya mateniti hospitalini hapo leo.

Inasemekana Rehema alibambwa na nesi wa zamu katika wodi hiyo ambaye ni mlokole, ambaye baada ya kuona mauzauza ya huyo msichana inasemekana alifanya maombi, na mtuhumiwa huyo akaanza kutambaa kama nyoka wodini hapo.

Polisi waliitwa na kumpeleka Rehema kituo kidogo kilichopo karibu na hospitali hiyo ambako alikiri kwamba yeye ni mtu wa juju, na kudai kwamba shughuli hiyo kafundishwa na bibi yake kwa jina la Salome Nganame.

Aliwaambia askari kwamba hakuwa peke yake katika skuli hiyo, kwani mafunzo hayo ya undondocha kafunzwa yeye na kinadada wengine aliowataja kama Asha Said(29), Fatuma Saleh(23) na Khadija Mpogolo.

Alisema yeye na hao aliowataja ilikuwa waibe pamoja mtoto pele hospitali na kwenda kumnyonya damu.

aliwaambia askari kwamba walipomkamata bibi huyo na wenzie walikuwa wanaw

acheki tu kwenye 'TV' yao huko waliko.Picha na Mpiga Picha Maalum wa TSN.

No comments: