Tuesday, June 03, 2008

Olusegun Obasanjo:

Ufisadi ni tatizo

kubwa Afrika

Nigerias Former President Olusegun Obasanjo


na Kulwa Karedia na Ramadhan Siwayombe, Arusha


RAIS mstaafu wa Nigeria, Olusegun Obasanjo, jana alitoa kauli nzito dhidi ya viongozi wa Afrika na kuwataka kupambana na rushwa katika nchi zao, hata kama zinawahusu viongozi wakuu waliopo madarakani na wale waliostaafu ndani ya nchi zao.

Obasanjo aliyasema hayo wakati akitoa nasaha katika siku ya kwanza ya mkutano wa nane wa Leon Sullivan, unaofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC), kabla haujafunguliwa na Rais Jakaya Kikwete jana jioni.

“Ili mataifa ya Afrika yaweze kupata maendeleo lazima viongozi wake wakubali kupambana na wala rushwa katika nchi zao, hata kama ni wakuu ndani ya nchi zao,” alisisitiza Obasanjo.


No comments: