Thursday, July 31, 2008

Wanawake wengi wa

Kitanzania waikana

nchi ili kuolewa nje



Na Ramadhan Semtawa, Dodoma

TAKWIMU za serikali kwa mwaka 2007/08 kuhusu taratibu za uraia zimetoka zikionyesha wanawake wa Kitanzania wanaongoza kwa kuukana uraia wao ili waolewe nje.

Akiwasilisha hotuba ya bajeti ya makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Mambo

ya Ndani kwa mwaka 2008/09, Waziri Lawrence Masha, alisema katika kipindi cha mwaka

2007/08 jumla ya Watanzania 63 waliukana uraia kati yao wanawake ni 50.

Masha alisema idadi hiyo ni sawa asilimia 74.9 ya walioukana uraia na kuongeza

kwamba wanaume walikuwa 13 sawa na asilimia 20.9.

Kuhusu idadi ya vijana wazamiaji nje, alisema kumekuwa na ongezeko la wazamiaji

hadi kufikia 382 mwaka 2007/8 kutoka 193 mwaka 2006/07.

Alisema wazamiaji hao vijana husingizia kwamba, wanakwenda kutafuta maisha bora




No comments: