Si kazi ya serikali
kuchuja habari
Na Joseph Mihangwa
MAPEMA mwezi huu makachero wa Jeshi la Polisi nchini walivamia na kupekua ofisi za gazeti hili na nyumbani kwa Mkurugenzi Mtendaji wake, Saed Kubenea, wakimtuhumu kuchukua akaunti za wateja wa Benki ya NBC na kuzichapisha katika gazeti lake.
Huu ni mtihani mwingine kwa uhuru wa vyombo vya habari nchini katika kipindi hiki kigumu cha taifa kuzama katika lindi la ufisadi, kuporomoka kwa maadili ya taifa na nchi kunyemelewa na ukoloni mamboleo.
Uhuru wa mawazo na wa kujieleza ni haki ya raia. Licha ya kwamba sehemu kubwa ya wajibu huu inatekelezwa na vyombo vya habari, vyombo hivi pia ni sauti ya wasio na sauti na waliofungwa midomo.
No comments:
Post a Comment