Safari za Kikwete
nje utata mtupu

Lula wa Ndali-Mwananzela
Tukiweka utani wote pembeni, kejeli zote pembeni, na dhihaka zote pembeni, bado tunakabiliwa na swali moja muhimu: Ni kwanini Rais Jakaya Kikwete hawezi kukaa Dar kwa angalau wiki tatu mfululizo bila kwenda nje ya nchi?
Hivi ni kweli kuwa bila Rais Kikwete kwenda safari za nje ya nchi Taifa haliwezi kuendelea na bila ya yeye mwenyewe kufunga safari hizo, basi, misaada ya kigeni na uwekezaji hautafanyika nchini kama alivyoashiria Waziri wa Mambo ya Nje, Bernard Membe, mapema mwaka huu?
Ninatatizwa, ninakerwa na niseme wazi kuwa baadhi ya ziara hizi haziingii akilini, na kwa hakika zinanifanya nianze kuhisi ninaishi katika ulimwengu wa kufikirika ambamo mambo yote yanawezekana.
No comments:
Post a Comment