Tuesday, November 25, 2008

Waziri Mkuu Pinda

asema: kuna

tatizo serikalini


Waziri Mkuu, Pinda


*Acharukia ma-RC, ma-DC, wakurugenzi 
*Asema migomo, maandamano ni kawaida 


BAADHI ya watendaji wakuu wa Serikali mikoani hadi wilayani ni dhaifu na ndicho chanzo cha matatizo yanayoikabili Serikali hivi sasa, imeelezwa. 

Hayo yalisemwa jana na Waziri Mkuu, Bw. Mizengo Pinda, alipokuwa alizungumza na wahariri wa vyombo vya habari ofisini kwake Dar es Salaam. 

Alisema usimamizi mbovu wa viongozi hao ndio umesababisha wananchi wasitatuliwe matatizo yao kwa wakati na hivyo kuleta migomo isiyokuwa na maana. 

"Baadhi ya wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya na wakurugenzi wa halmashauri zetu, wapo kusubiri mishahara tu, hawatusaidii kabisa," alisema Waziri Mkuu na kuwataka waondoke ofisini na kwenda kusaidia wananchi vijijini. 

No comments: