Waomba ukimbizi
hawatapewa vibali
vya kazi bila
utambulisho wa
kutoka wanakodai
wanatoka
Kuanzia sasa wanaokuja Norway kuomba hifadhi ya kikimbizi bila ya utambulisho wa wanakodai wanatoka, hawatapewa vibali vya kufanya kazi ya muda huku wakisubiri uamuzi wa kesi zao. Hayo yamesemwa na waziri wa kazi na majumlisho ya jamii, Bw. Dag Terje Andersen na kunukuliwa na gazeti la VG. Bw. Andersen ameiagiza idara ya wahamiaji (Utlendingsdirektoratet = UDI) kuwa kuanzia sasa wasiwe na mchezo wala huruma kwenye maamuzi ya kesi za wanaokuja bila vitambulisho/pasipoti.
Tisa kati ya kumi ya watu wanaokuja Norway kuomba hifadhi ya kikimbizi hawana aina yoyote ya utambulisho au pasipoti za wanakodai wanatoka, kutokana na takwimu za Idara Kuu ya Takwimu (Statistics Norway)
Mwanzoni wote waliokuwa wanakuja kuomba hifadhi ya kikimbizi walikuwa wanapewa vibali vya kufanya kazi huku wakisubiri uamuzi wa kesi zao.
No comments:
Post a Comment