Friday, April 30, 2010
Waombaji ukimbizi kwa utaifa
Kuna mdau mmoja msomaji wa blogu hii ameomba tafsiri ya ”Asylum application by nationality” kwa Kiswahili. Ifuatayo hapo chini ni tafsiri ya mhariri. Mhariri anaomba kumradhi kama tafsiri hii haijitoshelezi. Takwimu zilizopo kwenye hivyo viungo hapo chini ni idadi ya waombaji na nchi walizotoka. Ni matumaini kuwa halitakuwa tatizo kubwa kwa aliyeomba itafsiriwe kwa Kiswahili.
********************************************
Mwombaji ukimbizi ni mtu ambaye kwa hiari yake mwenyewe kaja na kuomba hifadhi hapa Norway. Kwa mujibu wa kanuni za haki za wakimbizi za Umoja wa Mataifa za mwaka 1951 na sheria za nchi hii, Norway inawajibika kuwalinda wote ambao kwa sababu za imani zao za kidini, utaifa, itikadi za kisiasa au kuwa mwanachama wa kundi la kijamii linaloonewa, kuamua kukimbia na kuja kuomba hifadhi ya ukimbizi.
Bofya na fungua viungo hapo chini – orodha ya watu kutoka nchi mbalimbali walioomba hifadhi:
- waombaji kwa utaifa 2010, 1.Januar-31.Machi.
- waombaji kwa utaifa mwaka 2009
- waombaji kwa utaifa mwaka 2008
- waombaji kwa utaifa mwaka 2000 hadi 2008
Ubelgiji yapiga marufuku mabaibui
kwenye sehemu za umma Bunge la Ubelgiji jana lilipiga kura na kupitisha sheria ya kupiga marufuku uvaaji wa Niqab na Burka (mabaibui) kwenye sehemu za umma. Wabunge 136 walisema NDIYO na wawili walikataa kupiga kura.
Kukiuka sheria hiyo, mtu anaweza kupigwa faini kati ya Euro 15 hadi 25 (sawa na kroner za Kinorwejiani 118-196 au shilingi za Tanzania 26956.50 hadi 44927.50) au jela siku saba au faini na jela pamoja.
Thursday, April 29, 2010
Norway
Kesho Ijumaa tarehe
30 Aprili 2010
ni siku ya mwisho
ya kurudisha:
Taarifa kuhusu mapato
yanayostahili kutozwa kodi
“Income Tax Return = ITR.”
Angalia vizuri mapato yako,
madeni yanayostahili
kuingizwa kwenye
hizo taarifa, n.k.
Linganisha na fomu ya
kodi ya mapato,
tulizotumiwa mwanzoni
mwa mwaka,
kabla hujarudisha “ITR”
Saa 5.59 usiku (23.59 CET),
ni saa ya mwisho ya
kurudisha ”ITR”.
Unaweza kuirudisha
kieletroniki.
Angalia:
au kwa SMS na. 02111 kama tayari una nywila
(koda) toka skatteetaten.
maelezo ya ziada wapigie
simu na. 800 80 000
Kila la heri!!!
Sudan - General Omer Hassan Al-Bashir
The people of Sudan have re-elected Gen. Omer Hassan Al-Bashir as their President. Gen. Salva Kiir has also won with a landslide as President of Southern Sudan which will soon vote to secede. 10,114,310 valid votes were cast in the election that ended days back.
Full results below:
1. Omer Hassan Al-Bashir (National Congress Party) 68.24% - 6,901,694 votes
2. Yasir Arman (Sudan People’s Liberation Movement) 21.69% - 2,193,826 votes
3. Abdullah Deng Nhial (Popular Congress Party) 3.92% - 396,139 votes
4. Hatim Al-Sir (Democratic Unionist Party) 1.93% - 195,668 votes
5. Al-Sadiq Al-Mahdi (Umma Party) 0.96% - 96,868 votes
6. Kamil Idriss (Independent) 0.76% - 77,132 votes
7. Mahmood Ahmed Jeha (Independent) 0.71% - 71,708 votes
8. Mubarak al-Fadil (Umma Reform and Renewal Party) 0.49% - 49,402 votes
9. Munir Sheikh El-din Jallab (New National Democratic Party) 0.40% - 40,277 votes
10. Abdel-Aziz Khalid (Sudanese National Alliance) 0.34%- 34,592 votes
11. Fatima Abdel-Mahmood (Sudanese Socialist Democratic Union) 0.30% - 30,562 votes
12. Mohamed Ibrahim Nugud (COMMUNIST PARTY) 0.26% - 26,442 votes
SOUTH SUDAN PRESIDENTIAL ELECTIONS
2,813,830 valid votes cast
1. Salva Kiir (Sudan People’s Liberation Movement) 92.99% - 2,616,613 votes
2. Lam Akol (Sudan People’s Liberation Movement for Democratic Change) 7.01% - 197,217 votes
From Sudan Tribune
Full results below:
1. Omer Hassan Al-Bashir (National Congress Party) 68.24% - 6,901,694 votes
2. Yasir Arman (Sudan People’s Liberation Movement) 21.69% - 2,193,826 votes
3. Abdullah Deng Nhial (Popular Congress Party) 3.92% - 396,139 votes
4. Hatim Al-Sir (Democratic Unionist Party) 1.93% - 195,668 votes
5. Al-Sadiq Al-Mahdi (Umma Party) 0.96% - 96,868 votes
6. Kamil Idriss (Independent) 0.76% - 77,132 votes
7. Mahmood Ahmed Jeha (Independent) 0.71% - 71,708 votes
8. Mubarak al-Fadil (Umma Reform and Renewal Party) 0.49% - 49,402 votes
9. Munir Sheikh El-din Jallab (New National Democratic Party) 0.40% - 40,277 votes
10. Abdel-Aziz Khalid (Sudanese National Alliance) 0.34%- 34,592 votes
11. Fatima Abdel-Mahmood (Sudanese Socialist Democratic Union) 0.30% - 30,562 votes
12. Mohamed Ibrahim Nugud (COMMUNIST PARTY) 0.26% - 26,442 votes
SOUTH SUDAN PRESIDENTIAL ELECTIONS
2,813,830 valid votes cast
1. Salva Kiir (Sudan People’s Liberation Movement) 92.99% - 2,616,613 votes
2. Lam Akol (Sudan People’s Liberation Movement for Democratic Change) 7.01% - 197,217 votes
From Sudan Tribune
Mraba wa Maggid kwenye Raia Mwema
Kudumisha Kiswahili ni kudumisha utamaduni wetu
HATUA ya hivi karibuni ya Serikali kutoka waraka wenye kutaka Kiswahili kitumike katika shughuli mbalimbali za kitaifa ni ya kupongezwa.
Juhudi zozote zile za kuitangaza, kuikuza na kuilinda lugha ya Kiswahili ni juhudi za kuulinda utamaduni wetu. Hakika inahusu utamaduni. Na utamaduni ni utaratibu wa maisha ikiwa ni pamoja na sanaa za maonyesho, muziki asilia, ngoma za asili, tamthilia, lugha, sanaa za ufundi, filamu na chakula. Utamaduni ni utambulisho wa mtu husika.
Tuna kila sababu ya kujikita katika kurejesha heshima, hadhi, moyo na juhudi za kukuza utamaduni wetu unaotishiwa kumezwa na tamaduni za kighaibu hususan zile za kimagharibi. Tutumie utandawazi unaoambatana na sayansi na teknolojia kama nyenzo na fursa ya mafanikio ya jitihada za kuendeleza, kukuza, kusambaza na kuuza utamaduni wetu.
Tuuthamini, kuuendeleza na kuukuza utamaduni wetu.
Leo ukisikiliza muziki unaopigwa kwenye redio zetu, filamu zinazonyeshwa na hata kuigizwa na Watanzania wenzetu. Ukiangalia aina ya mavazi tunayovaa, vyakula tunavyokula na hata lugha tunayozungumza. Vyote hivyo havitoi taswira ya utamaduni halisi wa Mtanzania. Maeneo ya mijini ndiyo yanayoelekea kumezwa zaidi na tamaduni za kighaibu.
Tuna haja ya kutafakari kwa kina juu ya utamaduni tunaoujenga sasa. Itakumbukwa, miaka ile ya mwanzoni mwa uhuru wetu, masuala ya utamaduni yaliwekwa chini ya Wizara ya Utamaduni wa Taifa na Vijana. Wizara hii ilianzishwa kwa mara ya kwanza mwaka 1962. Kunako Desemba 10, mwaka 1962, Mwalimu Nyerere aliweka bayana majukumu ya Wizara ya Utamaduni wa Taifa na Vijana, Mwalimu alitamka yafuatayo; " Mabadiliko makubwa niliyoyafanya ni kuanzisha Wizara mpya ya Utamaduni wa Taifa na Vijana. Nimefanya hivyo kwa kuamini kuwa Utamaduni ni kitu muhimu na ni roho ya taifa lolote liwalo.
Taifa lisilo na utamaduni ni sawa na mkusanyiko wa watu walikosa ari na moyo wenye kuwafanya kuwa taifa. Moja ya dhambi kubwa ya wakoloni ni ile hali ya kutufanya tuamini kuwa hatuna utamaduni wetu wa asili; au kwamba yote tuliyokuwa nayo hayakuwa na thamani yoyote-kitu ambacho tulipaswa tukionee aibu badala ya kuwa chanzo cha kujivunia.
Baadhi yetu, hususan wale tulioelimishwa na Wazungu tunanajaribu kuwathibitishia wakoloni waliotutawala kwamba "tumestaarabika" ikiwa na maana tumeachana na yale yote yenye kutuunganisha na utamaduni wetu wa asili. Kwamba tumejifunza kuiga utamaduni wa Kizungu. Malengo ya vijana wetu hayakuwa kuwa Waafrika walioelimika bali kuwa Wazungu Weusi." Hayo ni maneno ya Mwalimu Nyerere mwaka 1962.
Bila shaka, Mwalimu Nyerere alikuwa ni mfano wa viongozi waliothamini na kuuenzi utamaduni wetu ikiwamo lugha ya Kiswahili. Leo tunashuhudia jinsi jamii yetu ilivyovamiwa na tamaduni za kighaibu. Ni dhahiri kuwa utamaduni unaimarika kwa kuiga yaliyo mazuri kutoka tamaduni nyingine. Lakini katika jamii yetu, tamaduni za kighaibu hususan kutoka Ulaya na Marekani zaelekea kukumbatiwa zaidi na wanajamii na hivyo basi kuhatarisha kuufifisha na pengine kuuangamiza utamaduni wetu.
Vijana wetu wanaona fahari zaidi kuimba na kucheza nyimbo na miziki ya kighaibu. Wanaona aibu kuimba nyimbo za Kiswahili. Nyimbo za makabila yetu kwa mfano Kinyamwezi, Kizaramo na nyinginezo za asili. Vijana wetu wanaona fahari kuongea Kiswahili kwa lafidhi ya Kiingereza.
Vijana wetu wengi wa siku hizi hawajawahi kusikia au hata kujaribu kucheza Gombe Sugu, Mganda, Mangala, Konge, Nyang'umumi, Kiduo, au Lele Mama. Hizi ni baadhi tu ya ngoma zetu za asili. Vijana wetu wengi hawajawahi kusikia au hata kujaribu kupiga vyombo vya muziki vya asili kama vile Marimba, Kilamzi, Ligombo au Imangala.
Na tuangalie ni jinsi gani tutaweza kuuhifadhi, kuuendeleza na kuuimarisha utamaduni wetu. Labda hapa kuna haja ya pekee ya kutoa mfano wa suala la matumizi ya lugha kwa vile ndio kitovu cha utamaduni. Kwa upande wetu ni lugha ya Kiswahili.
Hivi leo kuna wanaozungumza au kuandika kwa Kiingereza mahali ambapo asilimia 90 ya wasikilizaji au wasomaji ni wazungumzaji wa Kiswahili. Hiyo ni hali ya kutojiamini. Ni kubaki katika hali ya utumwa wa fikra. Je, wenye kufanya hivyo wana malengo ya kuwaonyesha "wakoloni" au "wafadhili" wa semina kwamba wao "wamestaarabika"? Au wanafanya hivyo ili kuwaridhisha wafadhili tu? (Rejea kauli ya Mwalimu Nyerere mwaka 1962 hapo juu). Kwa nini waandaaji wa semina wasitumie wakalimani kuwatafsiria wasio wazungumzaji wa Kiswahili ambao ni asilimia 10 tu ya kadamnasi. Hilo pia lingetengeneza ajira kwa baadhi ya Watanzania.
Suala la kujiamini ni suala la utambulisho. Binadamu hawezi kujiamini kama hana hakika ya utambulisho wake. Tujiulize; sisi ni nani? Hili ni swali gumu na la kifalsafa. Lakini ni swali lenye kuhitaji majibu ili tuweze kujenga msingi imara wa utamaduni wetu.
Katika kujibu swali la sisi ni nani? Hatuna budi kuiangalia historia yetu. Historia ni wakati, muda. Kihistoria jana ni sawa na zamani. Wahenga wetu walitafsiri muda kama mkusanyiko wa matukio ya zamani na sasa. Waliamini yaliyotokea zamani na yanayotokea sasa ndiyo yenye kusaidia kubashiri yatakayotea kesho. Yataamua mustakabali, hali ya baadaye.
Kuna tofauti ya zamani kidogo na zamani sana. Kuna tofauti pia ya sasa hivi na sasa, baadaye kidogo na baadaye sana. Hatuwezi kuyazungumzia ya “ zamani sana” bila kugusia mila, jadi na desturi za wahenga wetu. Mila, jadi na desturi, ni sehemu ya urithi na hazina walizotuachia wahenga. Ni jadi, mila na desturi hizo ndizo zilizojenga msingi wa Taifa hili la Tanzania.
Wahenga wetu waliishi kwa kujikimu na walitumia mbinu na maarifa mengi katika harakati za kuziendeleza jamii zao. Miongoni mwao kulikuwa na mabingwa wa uhunzi, uashi, tiba na mengineyo. Jamii haikusimama kama mlingoti, ilikuwa ikipiga hatua za kimsingi na za kimaendeleo.
Miongoni mwetu kuna wenye majina ya kujivunia na yenye kuonyesha nuru ya historia yetu, mathalan,majina kama, mhunzi, fundi, chuma na mengineyo. Majina hayo yametokana na shughuli za jadi zikionyesha kuwa wahenga walianzisha hatua za maendeleo ya kiteknolojia.
Tusisahau kuwa, kuna miongoni mwetu wenye majina yenye kuonyesha doa jeusi la historia yetu, ukiyasikia majina hayo yanakumbushia majonzi na huzuni kuu iliyowafika wahenga. Majina kama Mtumwa, Kitwana na Kijakazi, Majiyapwani na mengineyo. Ni majina muhimu yenye kubeba historia yetu katika kipindi kile cha biashara ya utumwa. Hiyo ni historia yetu. Utambulisho wetu unatokana na historia hiyo. Hatuwezi kujitenga wala kuikana historia yetu.
Tujivunie historia yetu na utamaduni wetu ikiwamo lugha ya Kiswahili.
Simu:
0754 678 252
Barua-pepe:
Blogu:
Wednesday, April 28, 2010
Norway
Asylum application by nationality
An asylum seeker is a person who, on his or her own initiative and without prior notification, asks the Norwegian authorities for protection and recognition as a refugee. Norway provides protection to those who are persecuted because of their religion, nationality, political opinions or membership in a particular social group, based on the 1951 United Nations Convention on the Status of Refugees and Norwegian legislation.
- Asylum applications by nationality 2010, 1.january-31.march.
- Asylum applications by nationality 2009
- Asylum applications by nationality 2008
- Asylum applications by nationality 2000-2008
UDI = Norwegian Directorate of Immigration
Norway
A record in voluntary returns
“It is gratifying to note that the measures we have taken to increase the number of voluntary returns appear to be working,” says Anne Siri Rustad, Head of Department in the Directorate of Immigration (UDI).
During the three first months of this year, 352 persons have returned home with the help of the Norwegian authorities and the International Organisation for Migration (IOM). This is the highest figure since the voluntary return programme commenced in 2002.
Financial support
The majority of those who chose voluntary return were from Iraq, Kosovo and Serbia. Citizens from these countries who return voluntarily receive NOK 10,000 in reintegration support. It is intended that the amount of NOK 10,000 per person shall contribute towards easing the initial period after return.
For persons from Iraq and Afghanistan there is a special return programme that includes more comprehensive financial support for reintegration in their home country.
Obligation to return
Asylum seekers who have received final rejection of their application for protection are under obligation to leave the country. If they fail to leave, the police will take care of transport and return. It is better for all parties if persons who have received final rejection of their applications take an active choice and return voluntarily with financial help and support. Those who are escorted out of the country by the police do not receive any financial support.
UDI = Norwegian Directorate of Immigration
Wanafunzi wa Chuo Kikuu Oslo
wafukuzwa kwa kukopi mitihani
Wanafunzi kumi na moja wa taasisi ya TEKNOHAMA (TEKNOlojia ya HAbari na MAwasiliano) ya Chuo Kikuu cha Oslo, wamefukuzwa chuo kwa kukopi mitihani kutoka kwa kwenye mitihani walioyofanya wenzao na iliyokuwa imewekwa kwenye mtandao jamii wa Facebook. Wengine wanne wanachunguzwa.
Wanafunzi hao walikuwa na mitihani ya kuandika nyumbani, wakakopi kutoka kwa wenzao na kuiwakilisha kama yao bila kujua kuwa kuna programu zinazoweza kugundua kama mwanafunzi amekopi toka kwenye mitandao.
Tuesday, April 27, 2010
Aliyemwua Malcolm X
aachiwa baada ya miaka 44
Malcolm X (Al Hajj Malik El Shabazz)
Thomas Hagan (69), aliyekuwa akijulikana kama Talmadge X Hayer, akiwa na umri wa miaka 22 mwaka 1965, ni mtu pekee aliyekubali kuwa ndiye aliyemwua Malcolm X (Al Hajj Malik El Shabazz) ameachiwa na bodi ya msamaha baada ya kutumikia kifungo cha miaka 20 hadi maisha. Alihukumiwa mwaka 1966 na wenzake wawili, Muhammad Abdul Aziz na Kahlil Islam, wote watatu wakiwa wanachama wa kikundi cha Kiislamu cha Waafrika Waamerika kijulikanacho kama Nation of Islam. Aziz na Islam wamekana katakata kuhusika na mauaji wa Malcom X, nao walifungwa maisha. Aziz alisamehewa mwaka 1985 na Islam mwaka 1987.
Malcom X alipigwa risasi na kuuawa alipokuwa akitoa hotuba kwenye ukumbi wa Audubon Ballroom mjini New York tarehe 21 Februari 1965, mbele ya mkewe Dr. Betty Shabbaz na watoto wake wanne.
Malcolm X alikuwa mwanachama wa Nation of Islam na akajitoa na kuanza kumlaumu kiongozi wao wakati huo, Elijah Muhammad kuwa ni mwongo, ndumilakuwili, mnafiki na punguani. Kujitoa kwa Malcolm X kutoka kwenye Nation of Islam kulimjengea maadui wengi, kiasi mwenyewe alianza kuhisi kuwa maisha yake yako hatarini.
Mwanzoni Malcom X alikuwa na itikadi kali sana kuhusu watu wengine, kiasi cha kuonekana kama mbaguzi wa rangi, lakini alibadili msimamo pale alipokwenda kuhiji Mekka. Alipokuwa Mekka alikutana na watu wa aina mbalimbali na kufunguka macho. Akabadili jina na kujiita Malik El Shabazz.
Muda mrefu Thomas Hagan amekuwa akiomba kusamehewa, lakini amekuwa akikataliwa. Mara ya mwisho alipoomba alipewa sharti la kutafuta kazi na kuwa nayo kwa muda mrefu, kupimwa kuangalia kama hatumii madawa. Amekuwa akifanya kazi nje kwa miaka saba sasa na amesoma akiwa jela hadi kuchukua shahada ya uzamili ya sosholojia. Anasema bado ni mwislamu lakini si mwanachama wa Nation of Islam. Hagan amefurahi kuwa huru na kusema kuwa atatumia muda mwingi aliobaki nao kuwa pamoja na watoto wake, wenye miaka 21, 17, 14 na 10.
Sweet and sour Kikwete:
The two sides of
Tanzania’s president
President, Jakaya Kikwete "Jay Kay"
By ELSIE EYAKUZE, The East African
With the general elections set for October, Tanzanians are asking themselves what kind of Head of State have we subjected ourselves to in President Jakaya Kikwete - popularly referred to as Jay Kay.
Whatever reasons drove us to vote him into power with an overwhelming majority in 2005, we have had a decent period of time to observe him as an individual and test the mettle of his leadership.
There are probably as many opinions about President Kikwete as there are citizens.
Certainly in the course of informally surveying people, statements have ranged from complete dismissal through to fierce loyalty.
Not that Jay Kay is a polarizing figure mind you, it is just that if three Tanzanians are debating a political issue you will get at least five-and-a-half opinions out of them.
I myself am a sympathizer: many little boys- and a few brave little girls- imagine that they will one day be President, but very few have what it takes to make it happen.
Like all Tanzanian presidents bar Julius Nyerere, Jay Kay comes from a rather humble background, ergo he is closer to Obama than George W. Bush on the individual agency/intellect scale.
Since the ruling party Chama Cha Mapinduzi (CCM) is going to be launching its marketing, sorry, election campaign soon along with a detailed enumeration of their 'successes,' as perceived by themselves, I will focus on the broader things that this President and his administration have handled well:
1. Firing people in high places: Former Prime Minister Edward Lowassa, the late Governor of the Central Bank Daudi Ballali, Former Minister and one-time Attorney General Andrew Chenge, a number of hapless District Commissioners and the rest of the smug untouchables who have been canned within the past three years can attest: that loud whoosh was the sound of political elites’ impunity flying out the window. There is something to be said for setting such a deeply satisfying precedent. One day we might even find someone guilty of corruption, but let me not get ahead of myself.
- Hiring good people: The current Prime Minister, Mizengo Pinda is a decent lifetime civil servant. Chief Justice Augustino Ramadhani, Tanzania Broadcasting Corporation head Tido Mhando, national football team Taifa Stars coach Marcio Maximo- all of them seasoned professionals who have been recruited, promoted, sometimes relocated in order to shore up important institutions.
And these are a just a few of the easily visible ones. Considering his vast powers of appointment Jay Kay seems to be gunning for good lieutenants rather than simply rewarding his puppets, campaign funders, political allies and other presidential hangers-on. Although, naturally, he must do that too.
- Doing his bit for democracy: Vain he might be, but Jay Kay is not driven by the egotistical Bigmanism that continues to plague so many African heads of state. His occasional tantrums seem to be reserved for instances of incompetence that waste his time, such as lapses in protocol at State House events.
He generally faces vocal opposition and criticism with equanimity. This has served to set an excellent tone: within reasonable boundaries, Tanzanians can happily cast aspersions all over the government.
We obviously take advantage of this, especially in the blogosphere. Since so much of democratic discourse relies on intelligently vocal malcontents, things are slowly looking up for us and for civil society. At heart, I suspect that Jay Kay genuinely believes in this whole public service, will-of-the-people business. True democrats are a rare breed.
-Jay Kay and his youthful crew of flyboys (ministers and various other minions) have glamorized politics. I know that this is in keeping with our image-conscious, popular media-driven age. Fleets of State House BMWs, billboards with His Grinning Beauteousness smiling down at us at major intersections, politicians getting overly dramatic in Parliament...where is the decorum? I can't help but feel nostalgic for the stodgier times of yore when Tanzanian politicians had to keep it simple. At least we were spared the hysterics.
- The corruption problem. Jay Kay was in President Mkapa's cabinet as Minister for Foreign Affairs for a decade before he became President, so all the fishy deals and grand corruption cases that we are grappling with at present happened when he was in government. There are all kinds of implications in that, and naturally this weakens the credibility of his anti-corruption campaign.
- He travels all the time. All the time. Dear international community: stop sending Jay Kay invitations to receive honorary degrees, visit obscure Tanzanians Abroad societies, have a fireside chat about securing more aid, toodle around factories, examine the charms of Jamaican treetop tours or whatever else you have in mind. He can't resist them.
The man has itchy feet but it is costing us money and we need our President at home. Besides, our poor Minister of Foreign Affairs, Bernard Membe, is languishing in relative boredom and obscurity. Surely he could handle at least two or three of those donor-tickling trips per quarter.
There are more issues to wade through but those are the main points for now. To summarize, Jay Kay is a good fit for this stretch of Tanzania’s political journey: a free-marketeer with a redistributive philosophy, a technophilic democrat, a fierce patriot, a canny executive and a patient, dedicated, opportunistic man of ambition who lacks the predatory instincts that make the Putins of this world so creepy.
While I don't doubt that there are smarter, tougher, more sociopathic men out there who would make “better” leaders (read: more effective despots), Jay Kay is at worst inoffensive and at best very useful. This is not a bad range within which to work for a young African democracy.
Elsie Eyakuze is a Tanzanian blogger and media consultant. This piece was adapted from a post on her blog, The Mikocheni Report: http://mikochenireport.blogspot.com
Ray C mabalaa hayamwishi!
Kama ulikuwa na imani kwamba staa wa Bongo Fleva, Rehema Chalamila ‘Ray C’ anaishi raha mustarehe kwenye makazi mapya, anza kudai kiingilio, kwani siri zilizomo ndani ya mjengo huo wa ghorofa kwa sasa zipo nje.
Kabla ya Ray C kuhamia kwenye mjengo huo wa ghorofa, uliopo Sinza, Dar, mwanamuziki huyo alikumbwa na mikasa kadhaa, kama vile kuishi gesti, kutupiwa vitu nje na wifi yake na kutuama kwenye nyumba isiyo na kiwango chake.
Ijumaa Wikienda a.k.a The Biggest IQ Paper halina cha kupoteza kwa kuiweka hadharani kesi inayomkabili Ray C ya kupata mali kwa njia ya udanganyifu ambayo amefunguliwa na ‘mdada’ aliyempangisha hapo.
Gazeti hili limebaini kuwa Ray C amefunguliwa madai hayo kwenye Kituo cha Polisi Urafiki, Dar es Salaam chini ya kesi iliyohifadhiwa kwenye kitabu cha kumbukumbu za jeshi (Riport Book au RB) kwa namba URP/RB’3665/10 KUPATA MALI KWA NJIA YA UDANGANYIFU.
Katika kesi hiyo, inaelezwa kuwa mdai ambaye ni Agnes Edward Kasango alimkopesha Ray C mapazia yenye thamani ya shilingi 320,000 lakini mpaka leo hajalipwa pesa zake.
Inaelezwa kuwa Agnes alikuwa akiishi kwenye mjengo huo wa ghorofa ambao Ray C anaminya kwa sasa na alimuachia kwa makubaliano maalum.
Kutokana na madai hayo, gazeti hili lilimtafuta Agnes ambaye alipopatikana alikiri kumfungulia mashtaka Ray C na kuongeza kwamba amelazimika kufanya hivyo baada ya kuhangaika kwa muda mrefu kupata pesa zake bila mafanikio.
“Unajua mimi ndiye nilimpangisha Ray C nyumba anayokaa, kwahiyo wakati anaingia akaniomba nimuachie mapazia lakini mpaka leo pesa zangu hajanipa,” alisema Agnes na kuongeza:
“Ray C namdai pesa nyingine za kodi ya nyumba shilingi 400,000 lakini nazo ananizungusha kunipa.”
Akijibu maswali ya mwandishi wetu, Agnes alisema kuwa yeye alipanga kwenye nyumba hiyo kwa mkataba wa mwaka mzima na aliingia makubaliano na Kampuni ya Agumba Computers ambayo ndiyo yenye mamlaka.
“Niliishi miezi minne nikapata safari ya kwenda Afrika Kusini. Akaja Ray C, mimi nilikuwa simjui ila rafiki yangu anamjua. Akaniomba nimuamini. Sehemu niliyopanga ni ghorofani, kuna chumba kimoja cha kulala, choo, bafu na jiko.
“Basi nikazungumza na mwenye nyumba akaniruhusu nikubaliane na Ray C. Kutokana na mahesabu ya miezi saba na siku 10, akatakiwa kunilipa shilingi 2,500,000.
“Akaniomba nimpunguzie mpaka tukakubaliana shilingi 2,300,000. Akalipa 1,900,000 ‘keshi’ akaahidi kunimalizia 400,000 baada ya wiki mbili. Tulipokubaliana, nikampa na mkataba ambao niliingia moja kwa moja na mwenye nyumba.
“Hakunilipa kwa muda, nikasafiri kwenda Afrika Kusini, nikarudi, kila nikimuomba fedha zangu hanilipi kwa sababu jumla sasa ni shilingi 720,000, yaani 400,000 iliyobaki kwenye kodi ya nyumba na 320,000 ya mapazia,” alisema Agnes na kuongeza:
“Baada ya kuona ananisumbua ndiyo nimekwenda kumfungulia mashtaka, namdai mapazia yangu, halafu baadaye nitamfungulia mashtaka kuhusu 400,000 ya nyumba.”
Gazeti hili lilifanikiwa kuona hati ya makubaliano kati ya Ray C na Agnes ambapo mashahidi wawili wameanguka sahihi.
Mashahidi hao ni Fanny Ng’ambi kwa upande wa Agnes na Isaac Waziri Maputo ‘Lord Eyez’ kwa Ray C.
Aidha, katika hati hiyo ambayo inaonesha iliandikwa Oktoba 28, 2009, pia Ray C na Agnes kila mmoja ameanguka sahihi yake.
Jitihada za gazeti hili kumpata Ray C hazikuzaa matunda ila uchunguzi wa The Biggest IQ Paper, umeweza kupata uthibitisho ndani ya Kituo cha Polisi Urafiki kwamba mwanamuziki huyo anasakwa kwa tuhuma hizo.
Global Publishers Ltd (TZ)
Norway's Stoltenberg receives
Russian President Medvedev
Bilateral trade relations are central when Russian President Dmitry Medvedev visits Norway. On 26 April the President participates with Prime Minister Jens Stoltenberg at a major Norwegian-Russian trade and industry conference in Oslo.
"I am certain that President Medvedev's state visit to Norway will stimulate the further development of Norwegian-Russian trade and industry relations," says the Prime Minister.
The aim of the trade and industry conference is to demonstrate the broad scope and future possibilities for Norwegian-Russian trade and industry relations. Central topics are energy, fisheries, new technology and industrial cooperation. Central Norwegian and Russian trade and industry leaders will have the opportunity to meet with Stoltenberg and Medvedev.
Good working conditions are central to the development of Norwegian-Russian trade and industry relations. Russian membership in the WTO and the possibility of a future EFTA trade agreement with Russia will contribute to this. These will be central topics during the visit.
"A trade agreement between the EFTA countries and Russia has high priority for Norway, and we support Russian membership in the WTO," says Stoltenberg.
Russia is a central trade partner for Norway. In 2009 the total export to and import from Russia reached NOK 12 billion. Seafood represents more than 80 per cent of Norway's export to Russia. Over the last decade an increasing number of Norwegian companies have engaged in relations with Russia, and more than 100 companies now have permanent representation in Russia.
From the Prime Minister Office.
Subscribe to:
Posts (Atom)




.jpg)


