Saturday, September 03, 2011

Stavanger, Norway

50 Cent akutana na vijana waliopona kwenye
kisiwa cha Utoya


50 Cent akizungumza na kiongozi wa AUF, Eskil Pedersen baada ya konseti mjini Stavanger.


Alhamisi wiki hii mwanamziki wa kizazi kipya (Hip Hop/Rap) 50 Cent alitumbuiza kwenye tamasha la Rått na Råde mjini Stavanger. Baada ya tumbuizo lake, 50 Cents aliomba kukutana na vijana wa chama cha vijana cha Labour Norway cha AUF, waliopona kwenye mauaji ya Julai 22 ya vijana wa AUF kwenye kisiwa cha Utoya. 50 Cent pia alizungumza na kiongozi wa AUF; Eskil Pedersen (24). 50 Cent aliwaambia vijana hao wa AUF kuwa yuko nao pamoja kwani amekuwa akifuatilia kwa makini  tukio la ulipuaji wa majengo ya serikali Oslo na la mauaji ya Utoya. Aliwaambia pia kuwa yeye mwenye aliwahi kupigwa risasi mara 9 mwaka 2001 na kupona hivyo basi ana hisia na uchungu nao hao vijana.

No comments: