Molde FK mabingwa wa soka wa Norway
Timu ya soka ya Molde FK
imenyakua ubingwa wa soka ligi kuu ya Norway jana baada ya kutoka sare na
Strømgodset ya Drammen 2-2.
Molde FK imenyakua ubingwa kwa
kumalizia na pointi 55, wakati mshindi wa pili; Tromsø wamemalizia na pointi 47
na Rosenborg ya tatu na pointi 46.
Hii ni mara ya kwanza katika
historia ya Molde kuwa mabingwa wa soka hapa Norway. Molde katika msimu huu
ulioisha jana imekuwa ikifundishwa na mchezaji wa zamani wa Manchester United;
Ole Gunnar Solksjær.
No comments:
Post a Comment