Aftenposten:
licha
ya hela za misaada kupotelea kwa wajanja;
Norway
yamwaga mahela Tanzania.
Habari hizi zimeandikwa
kwenye gazeti la Jumamosi 29 Oktoba 2011 la Aftenposten (ukurasa wa 23, 23, 25,
26 na 27), zikiwa na kichwa cha habari “Verden sett fra Tanzania”
Wakati
Norway inafanya majadiliano na Serikali ya Tanzania juu ya kurudishwa mamilioni
ya hela za misaada yaliyopota bila kujulikana; Waziri wa misaada wa Norway; Bw.
Erik Solheim amwaga kroner milioni 500 kwa Tanzania kwenye mradi ulioanzishwa na
Umoja wa mataifa kuungwa mkono na waziri mkuu wa Norway; Bw. Jens Stoltenberg
uitwao “REDD – Reducing Emissions for Deforestation Degradation. Nchi ambazo
zitanufaika sana na REDD ni Brazil, Tanzania, Indonesia, Guyana, Mexico na
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).
Kwenye mradi uitwao “Management
of Natural Resources Programme (MNRP)” Norway ilitoa kroner milioni 300. Hela
hizo zilitolewa katika kipindi cha mwaka 1994-2006. Novemba 2006; Brian Cooksey
alitoa ripoti ya miaka 12 ya misaada nchini Tanzania ambayo ilionyesha kuwa
kulikuwa na utata na kupingana na ripoti zilizokuwa zikitolewa na Wizara ya
Mali Asili na Utalii. Cooksey aliona utata wa ripoti ya wizara hasa kwenye
mradi kwenye kisiwa cha Mafia (MIMP). Mwezi Mei 2007 ripoti ya mwisho kuhusu
mradi kwenye kisiwa cha Mafia, ulifichua ufisadi wa mradi huo; kuwa kuna mahela
kibao yameliwa. Mkaguzi Mdenish Arthur F. Andreasen ndiye aliyetoa ripoti ya
ukaguzi hakiki ya mradi wa huo kuwa mahela yameliwa!
Pamoja na hayo yote; ya kuwa
Tanzania imekuwa ikipokea misaada mingi kutoka nchi za Magaharibi hususan
Norway na kuwa idadi kubwa ya misaada hiyo imekuwa ikipotea kwenye mifuko ya
wajanja; Aftenposten wanashangazwa na uamuzi wa waziri wa misaada; Bw. Erik
Solheim kuendelea kumwaga mahela nchini Tanzania.
1 comment:
Kazi kwelikweli mwisho na wenyewe watakasirika watulazimishe tuoane jinsia moja,pesa za jenga mahekalu dar!
Post a Comment