Saturday, January 07, 2012

Kibaka aiba iPhone akamatwa kwa kutumia “Find My iPhone”


Jamaa aliibiwa iPhone yake ana akawapigia polisi kuwa kaibiwa iPhone yake. Kwa kupitia “application” iitwayo “Find My iPhone” polisi hawakuwa na kazi ngumu ya kumkamata kibaka wa iPhone ya jamaa!

“Find My iPhone” ni app ambayo unaweza kuingia kwenye iPhone yako kupitia kwenye kompyuta, halafu ukawa unaweza kufuta programu zilizoko kwenye iPhone au kujua kwa uhakika kabisa wapi iPhone yako iko kwa kutumia ramani.

Tukirudi kwenye tukio hilo lililotokea Jumamosi ya leo, jamaa aliyeibiwa simkono (simu ya mkononi) aliwapigia polisi na kuwaambia kuwa kwenye iPhone yake kuna “Find My iPhone” na anajua wapi iko na angewaongoza polisi kwa mwizi huyo. Polisi walikubali kufuatana na jamaa huyo hadi hapo aliposema. Wakamkamata huyo kibaka na mfukoni kwake wakaikuta na kuthibitisha ni iPhone ya jamaa. Kibaka amechukuliwa na yuko lupango, hatima yake haijulikani.

Haya yamethibitishwa na na mkuu wa operesheni wa kituo cha polisi cha katikati ya mji wa Oslo, Bw. Tor Jøkling.

Mwamedi Semboja,
Oslo.

No comments: