Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho
Kikwete leo, Jumatatu, Mei 6, 2013, ameamua kukatiza ziara yake ya Kiserikali
nchini Kuwait ili kurejea nyumbani kutokana na tukio la shambulio la kigaidi la
mlipuko mjini Arusha ambako watu wawili wamefariki na 60 wamejeruhiwa.
Rais Kikwete aliyekuwa aondoke kesho kurejea nyumbani, kukatiza ziara
hiyo na anaondoka Kuwait City kurejea nyumbani mara moja ili kuwa karibu na
wafiwa pamoja na wale waliojeruhiwa katika shambulio hilo la kigaidi.
Miongoni mwa shughuli ambazo hazitafanyika sasa kutokana na uamuzi huo
wa Rais ni ziara ya kutembelea Kampuni ya Mafuta ya Kuwait katika eneo la
Ahmadi mjini Kuwait. Aidha, Rais hatahudhuria dhifa ya chakula cha jioni
ambacho alikuwa anaandaliwa na Waziri Mkuu wa Kuwait, Mheshimiwa Sheikh Jaber
Al Mubarak Al Hamad Al Sabah.
No comments:
Post a Comment