Monday, April 21, 2014

Kwa upande wake, Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship, Zachary Kakobe ametangaza kuungana na wanaodai Serikali ya Tanganyika na kuahidi kujenga ari na shauku ya kuhakikisha inarejeshwa.


ASKOFU KAKOBE;

Kwa upande wake, Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship, Zachary Kakobe ametangaza kuungana na wanaodai Serikali ya Tanganyika na kuahidi kujenga ari na shauku ya kuhakikisha inarejeshwa.

Akizungumza wakati wa ibada ya Pasaka iliyofanyika kanisani hapo jana, Askofu Kakobe alisema anafanya hivyo si kwa ushabiki ila ni kutokana na mipango ya Mungu, ambayo iliwezesha kuwapo kwa Tanganyika huru. Huku akishangiliwa na waumini wa kanisa hilo, Askofu Kakobe alisema wanaoidai Tanganyika katika Bunge la Katiba wapo sahihi na yeye anaungana nao na kuwa wanaopinga wamekosa hofu ya Mungu.

“Serikali ilitumia mamilioni ya shilingi kuadhimisha miaka 50 ya Uhuru, lakini wanashindwa kutamka uhuru wa nchi gani!” 

(Chanzo, Gazeti la Mwananchi, Jtatu - 21/04/2014)



No comments: