Monday, April 21, 2014

Askofu wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG), mjini Moshi, Kilimanjaro, Glorious Shoo amewatahadharisha wajumbe wa Bunge la Katiba kutotumia wingi wao bungeni kuzuia mabadiliko ya Katiba.


ASKOFU GLORIOUS SHOO;

Askofu wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG), mjini Moshi, Kilimanjaro, Glorious Shoo amewatahadharisha wajumbe wa Bunge la Katiba kutotumia wingi wao bungeni kuzuia mabadiliko ya Katiba.

Akizungumza katika ibada ya Jubilee ya miaka 75 ya kanisa hilo, Askofu Shoo alisema umefika wakati ambao Watanzania wanataka mabadiliko, hivyo wajumbe wa Bunge Maalumu wasitumie wingi wao kuzuia mabadiliko.

“Tusilazimishe kwa wingi wetu kuzuia mabadiliko kwa sababu ukweli tunaposema wingi wetu ni pale bungeni tu, lakini wingi wetu sisi tulioko nje tunasikia kelele nyingi zinazolazimisha mabadiliko naiomba Serikali izingatie hilo,” alisema Askofu Shoo.

“Watu wanaosoma nyakati, wanajua ukifika wakati wa mabadiliko hakuna anayeweza kuzuia na ukijaribu kuyazuia mabadiliko hayo yanakuja kukubadilisha wewe,” alisema Askofu Shoo.

(Chanzo, Gazeti la Mwananchi, Jtatu - 21/04/2014)




No comments: