
Mawaziri
wa Muungano
wamepotosha
*Yachachamalia kauli za Khatib na Sumari
Na Ramadhan Haji, Zanzibar
Na Ramadhan Haji, Zanzibar
WIZARA ya Fedha na Uchumi Zanzibar, imesema maelezo yaliyotolewa bungeni Dodoma hivi karibuni na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano, Bw. Muhammed Seif Khatib na Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi, Bw. Jeremiah Sumari ni ya upotoshaji yasiyo na ukweli wowote.
Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Wizara hiyo jana, ilisema Serikali ya Muungano haijawahi kutoa mgao wa misaada ya kibajeti inayopelekewa kwa njia ya mikopo kwa SMZ na badala yake mikopo hiyo imekuwa ikitolewa na Benki ya Dunia, Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) na washirika wengine wa maendeleo.
"Tunaomba msaada wenu vyombo vya habari ili kuelezea ukweli wa jambo hili, ambalo linaweza kupotosha wananchi kwa kuwa kilichosemwa na waheshimiwa hao hakiendani na ukweli wenyewe, ni vyema kutoa taarifa hii kwa umma ili kusahihisha taarifa zilizotolewa awali," ilisema taarifa hiyo.
No comments:
Post a Comment