Sunday, July 27, 2008

NASAHA ZA MIHANGWA



Joseph Mihangwa

Uongozi umeigeuza

nchi yetu

shamba la bibi


“DUNIA ni jukwaa (la michezo ya kuigiza) ambapo kila mmoja hucheza nafasi yake kwa zamu…” (William Shakespeare katika Mfanyabiashara wa Venice).

Utawala wa nchi ni jukwaa la mchezo wa kuigiza ambapo kila mtawala huingia na kutoka kwa zamu (kupokezana vijiti?) baada ya kuigiza sehemu yake; lakini nchi na watu ni wa kudumu .

Chini ya utawala mzuri au mbaya wanaonufaika au kuathirika ni nchi na wananchi. Ndiyo maana, kwa kutambua hili, Serikali na watawala wamewekewa mipaka ya kikatiba. Mfano, hapa kwetu, Katiba inatamka wazi kwamba, “… Wananchi ndio msingi wa mamlaka yote, na Serikali itapata madaraka na mamlaka yake yote kutoka kwa wananchi kwa mujibu wa Katiba” (ibara 8 (1) (a) ) ; na pia kwamba, “Serikali itawajibika kwa wananchi “ (Ibara 8 (1) (c)) .


No comments: