Tuesday, May 26, 2009

Red Bull yasimamishwa

Kuuzwa Ujerumani:

ina cocaine kiasi flani




Majimbo 6 nchini Ujerumani yamesimamisha uuzaji wa kinywani maarufu cha kuongeza nguvu kiitwacho Red Bull, baada ya kugundulika kina miligram 0.4% ya cocaine. Majimbo hayo ni:  Hesse, North Rhine-Westphalia, Thuringia and Rhineland-Palatinate. Uchunguzi ulifanywa kwenye jimbo la Nordrhein-Westfalens. Kiwango cha asilimia 0.4 kilichogundulika ni kidogo sana kwa madhara ya binadamu, lakini kutokana na sheria za Ujerumani, ni marufuku kinywani au chakula cha aina yoyote kuwa na madawa ya kulevya, msemaji wa wizara ya afya, wa jimbo la Thuringia, Bw. Thomas Schulz ameiambia Deutsche Welle.

 Red Bull ilikubaliwa mwezi Aprili kuingizwa na kuuzwa nchini Norway. Kwa muda mrefu ilikuwa imepigwa marufuku kuuzwa nchini Norway na kwa sababu ya umaarufu wake, watu walikuwa wakienda kuinunua nchini Sweden na kuja nayo Norway. 

No comments: